Javascript must be enabled to continue!
Uchambuzi wa Miktadha ya Kijamii na Mchango Wake katika Ujifunzaji wa Kiswahili kama Lugha ya Pili Nchini Burundi
View through CrossRef
Makala hii inahusu miktadha ya kijamii na mchango wake katika kujifunza Kiswahili kama lugha ya pili nchini Burundi. Muktadha wa kijamii huathiri ujifunzaji wa lugha ya pili kwa kuchochea mawasiliano ya kuongea, kukuza, na kuboresha matumizi halisi ya lugha katika mazingira ya kawaida (Ellis R., 2008). Hali hii ilimchochea mtafiti kufanya utafiti huu ili kubainisha miktadha ya kijamii iliyopo jijini Bujumbura na kuonesha mchango wake katika kujifunza Kiswahili kama lugha ya pili. Mbinu ya hojaji ilitumiwa kukusanya data. Aidha, mbinu ya usampulishaji tajwa ilitumika kuteua watoataarifa. Watoataarifa hao walikuwa wanafunzi 20 kutoka Chuo Kikuu cha Burundi, kiwango cha shahada ya awali. Nadharia ya Utamaduni Jamii iliyoasisiwa na Mwanasaikolojia Vygotsky (1978) iliongoza utafiti huu.
Matokeo ya utafiti huu yamebainisha kuwa miktadha ya kijamii ya kujifunza Kiswahili jijini Bujumbura ni soko, hospitali, zahanati, nyumbani, na kadhalika. Matokeo pia yalionesha kuwa miktadha hiyo inawawezesha wanafunzi kuingiza msamiati mpya, kukuza stadi za kusikiliza na kuzungumza. Inawawezesha pia, kuimarisha umilisi wa utamaduni na maarifa kuhusu fasihi. Serikali ya Burundi inaombwa kuchukua miktadha ya kijamii kama mikakati rasmi inayochangia kujifunza Kiswahili nchini. Mwisho, makala hii inapendekeza serikali ya Burundi iwezeshe walimu wa Kiswahili kufuatilia ujifunzaji wa Kiswahili wa wanafunzi nje ya darasa.
Title: Uchambuzi wa Miktadha ya Kijamii na Mchango Wake katika Ujifunzaji wa Kiswahili kama Lugha ya Pili Nchini Burundi
Description:
Makala hii inahusu miktadha ya kijamii na mchango wake katika kujifunza Kiswahili kama lugha ya pili nchini Burundi.
Muktadha wa kijamii huathiri ujifunzaji wa lugha ya pili kwa kuchochea mawasiliano ya kuongea, kukuza, na kuboresha matumizi halisi ya lugha katika mazingira ya kawaida (Ellis R.
, 2008).
Hali hii ilimchochea mtafiti kufanya utafiti huu ili kubainisha miktadha ya kijamii iliyopo jijini Bujumbura na kuonesha mchango wake katika kujifunza Kiswahili kama lugha ya pili.
Mbinu ya hojaji ilitumiwa kukusanya data.
Aidha, mbinu ya usampulishaji tajwa ilitumika kuteua watoataarifa.
Watoataarifa hao walikuwa wanafunzi 20 kutoka Chuo Kikuu cha Burundi, kiwango cha shahada ya awali.
Nadharia ya Utamaduni Jamii iliyoasisiwa na Mwanasaikolojia Vygotsky (1978) iliongoza utafiti huu.
Matokeo ya utafiti huu yamebainisha kuwa miktadha ya kijamii ya kujifunza Kiswahili jijini Bujumbura ni soko, hospitali, zahanati, nyumbani, na kadhalika.
Matokeo pia yalionesha kuwa miktadha hiyo inawawezesha wanafunzi kuingiza msamiati mpya, kukuza stadi za kusikiliza na kuzungumza.
Inawawezesha pia, kuimarisha umilisi wa utamaduni na maarifa kuhusu fasihi.
Serikali ya Burundi inaombwa kuchukua miktadha ya kijamii kama mikakati rasmi inayochangia kujifunza Kiswahili nchini.
Mwisho, makala hii inapendekeza serikali ya Burundi iwezeshe walimu wa Kiswahili kufuatilia ujifunzaji wa Kiswahili wa wanafunzi nje ya darasa.
Related Results
Uraia, Lugha na Haki za Kidijitali: umuhimu wa lugha katika harakati za kuondoa ukoloni katika teknolojia
Uraia, Lugha na Haki za Kidijitali: umuhimu wa lugha katika harakati za kuondoa ukoloni katika teknolojia
Purpose
Maneno mengi yanayohusu haki za binadamu na haki za kiteknolojia hayajatafsiriwa katika lugha ya Kiswahili. Kwa hivyo, wataalamu wa teknolojia na watetezi wa haki za kidiji...
Uamilifu wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Kimatumizi kwenye Kaunti ya Bungoma
Uamilifu wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Kimatumizi kwenye Kaunti ya Bungoma
Lugha ni chombo maalum katika ustawishaji na uimarishaji wa rasilimali za mwanadamu. Pia, ni wenzo unaohimili sera ambazo hulenga katika kutimiza matarajio ya kitaifa katika nchi y...
Visababishi vya Idadi Kubwa ya Wanafunzi wa Shule za Sekondari Nchini Uganda Kutochukua Somo la Kiswahili
Visababishi vya Idadi Kubwa ya Wanafunzi wa Shule za Sekondari Nchini Uganda Kutochukua Somo la Kiswahili
Katika makala haya, mtafiti anaeleza visababishi vya idadi kubwa ya wanafunzi katika shule za upili nchini Uganda kutochukua somo la Kiswahili. Wakati wa kupunguza idadi ya masomo ...
Ushairi WA Kiganda Unavyoweza Kuchangia Na Kuendeleza Ushairi WA Kiswahili Kimtindo Na Kimaudhui: Mfano WA Ufundishaji Nchini Uganda
Ushairi WA Kiganda Unavyoweza Kuchangia Na Kuendeleza Ushairi WA Kiswahili Kimtindo Na Kimaudhui: Mfano WA Ufundishaji Nchini Uganda
Wanafunzi wengi nchini Uganda wanachukulia utanzu wa ushairi wa Kiswahili kuwa mgumu na wanapata ugumu katika kujifunza ushairi wa Kiswahili. Ushairi wa Kiganda umekuwa unatendwa v...
Matumizi ya Kiswahili katika Mawasiliano na Uongozi wa Kidini katika Shule za Upili Nchini Kenya: Mfano wa Shule ya Wasichana ya Itigo
Matumizi ya Kiswahili katika Mawasiliano na Uongozi wa Kidini katika Shule za Upili Nchini Kenya: Mfano wa Shule ya Wasichana ya Itigo
Utafiti huu ulichunguza matumizi ya Kiswahili katika mawasiliano na uongozi wa kidini katika shule ya wasichana ya Itigo. Ulilenga kubaini jinsi lugha ya Kiswahili hutumika katika ...
Kuchambua Athari ya Vivumishi vya Runyakitara Katika Ujifunzaji wa Lugha ya Kiswahili Nchini Uganda
Kuchambua Athari ya Vivumishi vya Runyakitara Katika Ujifunzaji wa Lugha ya Kiswahili Nchini Uganda
Katika mfumo wa elimu nchini Uganda, Kiswahili ni lugha muhimu kwa mawasiliano na maendeleo ya kijamii. Hata hivyo, wanafunzi wanaozungumza Runyakitara wanakumbana na changamoto ka...
Matumizi ya Kiswahili katika Ujumuishaji wa Kidemokrasia kwenye Uchaguzi Nchini Tanzania
Matumizi ya Kiswahili katika Ujumuishaji wa Kidemokrasia kwenye Uchaguzi Nchini Tanzania
Makala haya yanaeleza matumizi ya lugha ya Kiswahili katika ujumuishaji wa kidemokrasia nchini Tanzania kwa kuzingatia matumizi ya lugha hiyo kwenye michakato ya uchaguzi. Lengo la...
Nafasi ya Ikolojia ya Lugha katika Mtagusano wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Dini katika Kaunti ya Bungoma
Nafasi ya Ikolojia ya Lugha katika Mtagusano wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Dini katika Kaunti ya Bungoma
Nyanja mbalimbali katika jamii hutegemea matumizi ya lugha. Hali hii huzua changamoto ya namna ya kutumia raslimali za lugha zinazopatikana katika jamiilugha fulani. Juhudi ya kufa...

