Search engine for discovering works of Art, research articles, and books related to Art and Culture
ShareThis
Javascript must be enabled to continue!

Matumizi ya Kiswahili katika Ujumuishaji wa Kidemokrasia kwenye Uchaguzi Nchini Tanzania

View through CrossRef
Makala haya yanaeleza matumizi ya lugha ya Kiswahili katika ujumuishaji wa kidemokrasia nchini Tanzania kwa kuzingatia matumizi ya lugha hiyo kwenye michakato ya uchaguzi. Lengo la makala haya ni kuonesha maeneo muhimu ya uchaguzi ambamo lugha ya Kiswahili inatumika, na kupendekeza mikakati inayoweza kufanikisha lugha hiyo kutumika zaidi katika masuala ya uchaguzi na kwenye michakato mingine ya ujenzi wa demokrasia Tanzania. Makala haya yanaakisi matumizi na mchango muhimu wa lugha ya Kiswahili katika michakato ya siasa za uchaguzi nchini Tanzania kama sehemu ya ujumuishaji wa kidemokrasia. Inaonesha kuwa katika michakato ya uchaguzi nchini Tanzania, lugha ya Kiswahili inatumiwa ili kufanya mawasiliano yanayoweza kuwajumuisha Watanzania wengi kwenye hatua mbalimbali za shughuli za uchaguzi. Makala haya yanatumia Nadharia ya Uchambuzi Kilongo. Nadharia hii inaeleza kuwa athari za matumizi ya lugha hazibaki kwenye eneo lake la matumizi pekee bali huvuka mipaka ya muktadha wa matumizi yake na kuathiri masilugha mengine. Makala haya yametumia data za upili ambapo nyaraka ngumu na laini zilizoandikwa kwa Kiswahili kuhusu shughuli za uchaguzi nchini Tanzania zilisomwa. Data za utafiti huu zimewasilishwa kwa njia ya maelezo. Matokeo ya utafiti uliozaa makala haya yanaonesha kwamba lugha ya Kiswahili inawawezesha Watanzania wengi kujumuishwa kwenye demokrasia ya uchaguzi kupitia michakato mbalimbali ambayo ni uandikaji wa matini tumizi ya uchaguzi, nyimbo za kampeni za uchaguzi, utangazaji wa matokeo ya uchaguzi, uapisho wa viongozi wateule, uandikaji wa ripoti ya uchaguzi na tathmini ya uchaguzi. Makala haya yanapendekeza kuwa matumizi ya lugha ya Kiswahili yaimarishwe zaidi kwenye michakato ya uchaguzi na kwenye michakato mingine ya kisiasa ili kujenga ujumuishi mpana wa kidemokrasia.
University of Dar es Salaam
Title: Matumizi ya Kiswahili katika Ujumuishaji wa Kidemokrasia kwenye Uchaguzi Nchini Tanzania
Description:
Makala haya yanaeleza matumizi ya lugha ya Kiswahili katika ujumuishaji wa kidemokrasia nchini Tanzania kwa kuzingatia matumizi ya lugha hiyo kwenye michakato ya uchaguzi.
Lengo la makala haya ni kuonesha maeneo muhimu ya uchaguzi ambamo lugha ya Kiswahili inatumika, na kupendekeza mikakati inayoweza kufanikisha lugha hiyo kutumika zaidi katika masuala ya uchaguzi na kwenye michakato mingine ya ujenzi wa demokrasia Tanzania.
Makala haya yanaakisi matumizi na mchango muhimu wa lugha ya Kiswahili katika michakato ya siasa za uchaguzi nchini Tanzania kama sehemu ya ujumuishaji wa kidemokrasia.
Inaonesha kuwa katika michakato ya uchaguzi nchini Tanzania, lugha ya Kiswahili inatumiwa ili kufanya mawasiliano yanayoweza kuwajumuisha Watanzania wengi kwenye hatua mbalimbali za shughuli za uchaguzi.
Makala haya yanatumia Nadharia ya Uchambuzi Kilongo.
Nadharia hii inaeleza kuwa athari za matumizi ya lugha hazibaki kwenye eneo lake la matumizi pekee bali huvuka mipaka ya muktadha wa matumizi yake na kuathiri masilugha mengine.
Makala haya yametumia data za upili ambapo nyaraka ngumu na laini zilizoandikwa kwa Kiswahili kuhusu shughuli za uchaguzi nchini Tanzania zilisomwa.
Data za utafiti huu zimewasilishwa kwa njia ya maelezo.
Matokeo ya utafiti uliozaa makala haya yanaonesha kwamba lugha ya Kiswahili inawawezesha Watanzania wengi kujumuishwa kwenye demokrasia ya uchaguzi kupitia michakato mbalimbali ambayo ni uandikaji wa matini tumizi ya uchaguzi, nyimbo za kampeni za uchaguzi, utangazaji wa matokeo ya uchaguzi, uapisho wa viongozi wateule, uandikaji wa ripoti ya uchaguzi na tathmini ya uchaguzi.
Makala haya yanapendekeza kuwa matumizi ya lugha ya Kiswahili yaimarishwe zaidi kwenye michakato ya uchaguzi na kwenye michakato mingine ya kisiasa ili kujenga ujumuishi mpana wa kidemokrasia.

Related Results

Uraia, Lugha na Haki za Kidijitali: umuhimu wa lugha katika harakati za kuondoa ukoloni katika teknolojia
Uraia, Lugha na Haki za Kidijitali: umuhimu wa lugha katika harakati za kuondoa ukoloni katika teknolojia
Purpose Maneno mengi yanayohusu haki za binadamu na haki za kiteknolojia hayajatafsiriwa katika lugha ya Kiswahili. Kwa hivyo, wataalamu wa teknolojia na watetezi wa haki za kidiji...
Ushairi WA Kiganda Unavyoweza Kuchangia Na Kuendeleza Ushairi WA Kiswahili Kimtindo Na Kimaudhui: Mfano WA Ufundishaji Nchini Uganda
Ushairi WA Kiganda Unavyoweza Kuchangia Na Kuendeleza Ushairi WA Kiswahili Kimtindo Na Kimaudhui: Mfano WA Ufundishaji Nchini Uganda
Wanafunzi wengi nchini Uganda wanachukulia utanzu wa ushairi wa Kiswahili kuwa mgumu na wanapata ugumu katika kujifunza ushairi wa Kiswahili. Ushairi wa Kiganda umekuwa unatendwa v...
Mabadiliko katika Mtaala wa Elimu ya Msingi na Namna Yanavyoathiri Tathmini katika Elimu ya Juu
Mabadiliko katika Mtaala wa Elimu ya Msingi na Namna Yanavyoathiri Tathmini katika Elimu ya Juu
Makala haya yamekusudia kuchunguza namna ambavyo mabadiliko katika mtaala wa elimu ya msingi yanavyoathiri tathmini katika elimu ya juu. Mabadiliko ya mtaala yanafanyika katika nga...
Uamilifu wa Mofu {(-)i-} katika Kiswahili Kinachozungumzwa nchini Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Uamilifu wa Mofu {(-)i-} katika Kiswahili Kinachozungumzwa nchini Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Makala hii inachunguza uamilifu wa mofu {(-)i-} katika Kiswahili kinachozungumzwa nchini Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Data zilizotumiwa zilikusanywa kutoka katika v...
Nafasi ya Ikolojia ya Lugha katika Mtagusano wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Dini katika Kaunti ya Bungoma
Nafasi ya Ikolojia ya Lugha katika Mtagusano wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Dini katika Kaunti ya Bungoma
Nyanja mbalimbali katika jamii hutegemea matumizi ya lugha. Hali hii huzua changamoto ya namna ya kutumia raslimali za lugha zinazopatikana katika jamiilugha fulani. Juhudi ya kufa...
Matumizi ya Lugha Kwenye Malezi ya Watoto: Mfano wa Matumizi ya Semi Katika Jamii ya Wamasaaba Nchini Uganda
Matumizi ya Lugha Kwenye Malezi ya Watoto: Mfano wa Matumizi ya Semi Katika Jamii ya Wamasaaba Nchini Uganda
Katika makala haya, mtafiti anaeleza jinsi lugha inavyotumiwa na wazazi katika shughuli yao ya kulea watoto. Alifanya hivyo kwa kurejelea malezi ya watoto katika jamii ya Wamasaaba...
Ubainishaji wa Vipengele vya Ujumi wa Kiafrika na Athari yake katika Ushairi wa Kiswahili: Uchunguzi wa Ushairi wa Bongo Fleva
Ubainishaji wa Vipengele vya Ujumi wa Kiafrika na Athari yake katika Ushairi wa Kiswahili: Uchunguzi wa Ushairi wa Bongo Fleva
Makala haya yalichunguza ujitokezaji wa ujumi wa Kiafrika katika ushairi wa Kiswahili wa Bongo Fleva pamoja na athari yake katika ushairi huo. Tafiti kuhusu vipengele vya ujumi wa ...
Uambikaji wa Viambishi Ngeli katika Nomino Sahili Zinazorejelea Ndugu na Maana yake katika Sarufi ya Kiswahili
Uambikaji wa Viambishi Ngeli katika Nomino Sahili Zinazorejelea Ndugu na Maana yake katika Sarufi ya Kiswahili
Nomino sahili ni maneno ambayo kimofolojia yameundwa na mofu huru moja. Pia, kisematiki, maneno haya yana maana zake katika kamusi. Licha ya kuwa na sifa hizi, uambikaji wa viambis...

Back to Top