Javascript must be enabled to continue!
Uraia, Lugha na Haki za Kidijitali: umuhimu wa lugha katika harakati za kuondoa ukoloni katika teknolojia
View through CrossRef
Purpose
Maneno mengi yanayohusu haki za binadamu na haki za kiteknolojia hayajatafsiriwa katika lugha ya Kiswahili. Kwa hivyo, wataalamu wa teknolojia na watetezi wa haki za kidijitali hutumia maneno ya Kiingereza – hata bila utohozi – wanapozungumzia haki za kiteknolojia. Hali hii ya mambo inachangia udhoofu fulani katika utetezi wa haki za kidijitali kwani wanaojaribu kueleza jamii umuhimu wa haki hizi hulazimishwa kutegemea msamiati wa Kiingereza usiyo na msingi au viungo na lugha ya Kiswahili Katika makala hii, tutazungumzia umuhimu wa kukaribisha watu kutumia lugha za Kiafrika kwenye mtandao.
Design/methodology/approach
Kiswahili ni lugha ya Kiafrika inayozungumzwa katika eneo zaidi sana duniani. Karibu watu milioni mia moja na arobaini Afrika mashariki wanazungumza Kiswahili kama lugha yao ya kwanza au ya pili, miongoni mwao Wakenya na Watanzania, wenyeji wa nchi ambamo Kiswahili ni lugha ya kitaifa. Tena kuna historia ndefu ya kutumiwa kwa lugha ya Kiswahili katika uandishi, uchapishaji na ubunifu wa utamaduni wa kisasa. Kiswahili pekee yake ndiyo lugha ya asili ya Kiafrika inayotumika kama lugha ya maalum ya Umoja wa Mataifa za Kiafrika. Hata hivyo, kwa upande wa matumizi ya Kiswahili, hasa kwenye mada ya teknolojia, Kiswahili imewachwa nyuma.
Findings
Zaidi ya maneno rasmi, uwepo wa lugha za Kiafrika ni muhimu kuimarisha jumuiya za Kiafrika mtandaoni kwani lugha inalenga sana haki na utambulisho wa watu. Miradi za kutafsiri maneno za kiteknolojia katika lugha ya Kiswahili inahimiza jumuiya za Afrika Mashariki kuunda jamii inayosimamia matakwa yao vyema. Makala hii basi inazingatia umuhimu wa lugha kwenye kuunda jamii na katika hatua za kuondoa mbinu za kikoloni mtandaoni ili wenyeji wa Afrika Mashariki wajione mtandaoni kwa ujumla wao wote. Makala pia itazingatia semiotiki ya lugha katika ubunifu wa teknolojia, na umuhimu wa kutafsiri jamii ya lugha ya Kiswahili katika harakati za kuondoa ukoloni katika ubunifu huu. Lakini sio tu kwamba lugha ya Kiswahili ndio pekee inayoweza kuondoa mbinu za kikoloni mtandaoni, kwani pia lugha hiyo ina ishara za kutawalwa kwa jamii fulani. Bali makala hii inatumia mfano wa Kiswahili kuhimiza utumiaji wa lugha za kiasili au za kimama mtandaoni ili kulinda mustakabali wa kidijitali wa umma.
Originality/value
Umuhimu wa makala hii ni kuashiria jipya umuhimu wa lugha katika harakati za kuendeleza haki za kidijitali na hasa kuondoa mbinu za kikoloni kwenye teknolojia, swala lisilowahijadiliwa katika lugha ya Kiswahili.
Title: Uraia, Lugha na Haki za Kidijitali: umuhimu wa lugha katika harakati za kuondoa ukoloni katika teknolojia
Description:
Purpose
Maneno mengi yanayohusu haki za binadamu na haki za kiteknolojia hayajatafsiriwa katika lugha ya Kiswahili.
Kwa hivyo, wataalamu wa teknolojia na watetezi wa haki za kidijitali hutumia maneno ya Kiingereza – hata bila utohozi – wanapozungumzia haki za kiteknolojia.
Hali hii ya mambo inachangia udhoofu fulani katika utetezi wa haki za kidijitali kwani wanaojaribu kueleza jamii umuhimu wa haki hizi hulazimishwa kutegemea msamiati wa Kiingereza usiyo na msingi au viungo na lugha ya Kiswahili Katika makala hii, tutazungumzia umuhimu wa kukaribisha watu kutumia lugha za Kiafrika kwenye mtandao.
Design/methodology/approach
Kiswahili ni lugha ya Kiafrika inayozungumzwa katika eneo zaidi sana duniani.
Karibu watu milioni mia moja na arobaini Afrika mashariki wanazungumza Kiswahili kama lugha yao ya kwanza au ya pili, miongoni mwao Wakenya na Watanzania, wenyeji wa nchi ambamo Kiswahili ni lugha ya kitaifa.
Tena kuna historia ndefu ya kutumiwa kwa lugha ya Kiswahili katika uandishi, uchapishaji na ubunifu wa utamaduni wa kisasa.
Kiswahili pekee yake ndiyo lugha ya asili ya Kiafrika inayotumika kama lugha ya maalum ya Umoja wa Mataifa za Kiafrika.
Hata hivyo, kwa upande wa matumizi ya Kiswahili, hasa kwenye mada ya teknolojia, Kiswahili imewachwa nyuma.
Findings
Zaidi ya maneno rasmi, uwepo wa lugha za Kiafrika ni muhimu kuimarisha jumuiya za Kiafrika mtandaoni kwani lugha inalenga sana haki na utambulisho wa watu.
Miradi za kutafsiri maneno za kiteknolojia katika lugha ya Kiswahili inahimiza jumuiya za Afrika Mashariki kuunda jamii inayosimamia matakwa yao vyema.
Makala hii basi inazingatia umuhimu wa lugha kwenye kuunda jamii na katika hatua za kuondoa mbinu za kikoloni mtandaoni ili wenyeji wa Afrika Mashariki wajione mtandaoni kwa ujumla wao wote.
Makala pia itazingatia semiotiki ya lugha katika ubunifu wa teknolojia, na umuhimu wa kutafsiri jamii ya lugha ya Kiswahili katika harakati za kuondoa ukoloni katika ubunifu huu.
Lakini sio tu kwamba lugha ya Kiswahili ndio pekee inayoweza kuondoa mbinu za kikoloni mtandaoni, kwani pia lugha hiyo ina ishara za kutawalwa kwa jamii fulani.
Bali makala hii inatumia mfano wa Kiswahili kuhimiza utumiaji wa lugha za kiasili au za kimama mtandaoni ili kulinda mustakabali wa kidijitali wa umma.
Originality/value
Umuhimu wa makala hii ni kuashiria jipya umuhimu wa lugha katika harakati za kuendeleza haki za kidijitali na hasa kuondoa mbinu za kikoloni kwenye teknolojia, swala lisilowahijadiliwa katika lugha ya Kiswahili.
Related Results
Nafasi ya Ikolojia ya Lugha katika Mtagusano wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Dini katika Kaunti ya Bungoma
Nafasi ya Ikolojia ya Lugha katika Mtagusano wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Dini katika Kaunti ya Bungoma
Nyanja mbalimbali katika jamii hutegemea matumizi ya lugha. Hali hii huzua changamoto ya namna ya kutumia raslimali za lugha zinazopatikana katika jamiilugha fulani. Juhudi ya kufa...
Mabadiliko katika Mtaala wa Elimu ya Msingi na Namna Yanavyoathiri Tathmini katika Elimu ya Juu
Mabadiliko katika Mtaala wa Elimu ya Msingi na Namna Yanavyoathiri Tathmini katika Elimu ya Juu
Makala haya yamekusudia kuchunguza namna ambavyo mabadiliko katika mtaala wa elimu ya msingi yanavyoathiri tathmini katika elimu ya juu. Mabadiliko ya mtaala yanafanyika katika nga...
Matumizi ya Lugha Kwenye Malezi ya Watoto: Mfano wa Matumizi ya Semi Katika Jamii ya Wamasaaba Nchini Uganda
Matumizi ya Lugha Kwenye Malezi ya Watoto: Mfano wa Matumizi ya Semi Katika Jamii ya Wamasaaba Nchini Uganda
Katika makala haya, mtafiti anaeleza jinsi lugha inavyotumiwa na wazazi katika shughuli yao ya kulea watoto. Alifanya hivyo kwa kurejelea malezi ya watoto katika jamii ya Wamasaaba...
Ujitokezaji wa Viarudhi vya Kifonolojia katika Kihaya: Uchunguzi Kifani wa Toni katika Lahaja ya Kihamba
Ujitokezaji wa Viarudhi vya Kifonolojia katika Kihaya: Uchunguzi Kifani wa Toni katika Lahaja ya Kihamba
Fonolojia ni taaluma iliyosheheni viarudhi au vipambasauti kama ambavyo wataalamu wengine huviita. Miongoni mwake ni toni, lafudhi, mkazo, nguvumsikiko, usilabi, kiimbo, unguvunguv...
Matumizi ya Lugha katika Tamthiliya ya ( Sadaka ya John Okello )
Matumizi ya Lugha katika Tamthiliya ya ( Sadaka ya John Okello )
Kipengele hiki hakipatikani katika lugha zote (bonyeza chache tu). Grafu iliyotangulia Ni ngapi huduma hii haipatikani katika lugha zote. Chini ni orodha ya kurasa zetu maarufu za ...
Ubainishaji wa Vipengele vya Ujumi wa Kiafrika na Athari yake katika Ushairi wa Kiswahili: Uchunguzi wa Ushairi wa Bongo Fleva
Ubainishaji wa Vipengele vya Ujumi wa Kiafrika na Athari yake katika Ushairi wa Kiswahili: Uchunguzi wa Ushairi wa Bongo Fleva
Makala haya yalichunguza ujitokezaji wa ujumi wa Kiafrika katika ushairi wa Kiswahili wa Bongo Fleva pamoja na athari yake katika ushairi huo. Tafiti kuhusu vipengele vya ujumi wa ...
Mchango wa Mikakati ya Upole Katika Mazungumzo ya ibada ya Mazishi katika Lugha ya Kikabrasi
Mchango wa Mikakati ya Upole Katika Mazungumzo ya ibada ya Mazishi katika Lugha ya Kikabrasi
Swahili
Suala la upole limetafitiwa na wasomi wengi kwenye mawasiliano, ikiwemo mazungumzo ya abiria na wahudumu wa magari ya uchukuzi kwa lugha ya Kikamba. Hata hivyo, utafiti huu...
Kupambanua Mbinu za Uwakilishi wa Uhalisia-Ajabu Katika Mustakabali wa Uongozi Barani Afrika Katika Karne ya 21 Katika Riwaya ya Babu Alipofufuka.
Kupambanua Mbinu za Uwakilishi wa Uhalisia-Ajabu Katika Mustakabali wa Uongozi Barani Afrika Katika Karne ya 21 Katika Riwaya ya Babu Alipofufuka.
Sanaa za kihalisia-ajabu husheheni usimulizi wa matukio yasiyotafsirika wala kufikirika kuwa na uyakinifu katika maisha ya mwanadamu. Fasihi za aina hii hutilia nguvu umazingaombwe...

