Search engine for discovering works of Art, research articles, and books related to Art and Culture
ShareThis
Javascript must be enabled to continue!

Matumizi ya Lugha Kwenye Malezi ya Watoto: Mfano wa Matumizi ya Semi Katika Jamii ya Wamasaaba Nchini Uganda

View through CrossRef
Katika makala haya, mtafiti anaeleza jinsi lugha inavyotumiwa na wazazi katika shughuli yao ya kulea watoto. Alifanya hivyo kwa kurejelea malezi ya watoto katika jamii ya Wamasaaba nchini Uganda. Kwa kurejelea jamii hii, mtafiti alieleza namna wazazi wanavyotumia lugha kulea watoto wao.  Alifanya hivyo kwa kunukuu baadhi ya semi ambazo zinasemekana zinatumiwa na wazazi katika shughuli ya kulea watoto. Ni kweli kwamba lugha yoyote ile hufanya kazi nyingi sana kama vile kutumbuiza watu, kuficha siri, kuseng’enya watu, kuibia watu, kutongozana, kushawishi, kugombana, kujitetea, kufundisha, nakadhalika. Hii ni kwa sababu bila kutumia lugha, mtu hawezi akaimba, akagombana, akaiba kwa kudang’anya, akafundisha, akaseng’enya, akatongoza, n.k. Hata hivyo, katika makala haya, mtafiti alijikita kwenye malezi ya watoto. Katika kazi hii, mtafiti alizingatia semi mbalimbali ambazo Wamasaaba huzitumia kwa ajili ya kuwaelekeza watoto wao ili wasije wakatenda maovu ukubwani. Katika jamii mbalimbali, watu hutumia lugha kutekeleza jambo hili. Jamii hasa zile za jadi zilitumia lugha kuwaelekeza watoto wao. Kuna namna ambavyo walisuka lugha kisanaa kwa lengo la kufunza watoto wao. Hii ni kwa sababu hawakuwa na madarasa maalumu mwa kufunzia watoto wao kama ilivyo sasa. Katika jamii hizo, shule zenyewe hazikuwepo. Kwa hiyo, lugha ndiyo ilikuwa chombo maalumu cha kufunzia watoto. Matumizi ya lugha yalidhamiria kukuza watoto wenye tabia nzuri. Hii ni kwa sababu watoto wenye tabia mbaya waliletea wazazi wao aibu. Hivyo basi, katika kazi hii, mtafiti alijikita katika matumizi ya lugha na kueleza jinsi Wamasaaba wanavyotumia semi mbalimbali kuelekeza watoto wao kitabia.
East African Nature and Science Organization
Title: Matumizi ya Lugha Kwenye Malezi ya Watoto: Mfano wa Matumizi ya Semi Katika Jamii ya Wamasaaba Nchini Uganda
Description:
Katika makala haya, mtafiti anaeleza jinsi lugha inavyotumiwa na wazazi katika shughuli yao ya kulea watoto.
Alifanya hivyo kwa kurejelea malezi ya watoto katika jamii ya Wamasaaba nchini Uganda.
Kwa kurejelea jamii hii, mtafiti alieleza namna wazazi wanavyotumia lugha kulea watoto wao.
  Alifanya hivyo kwa kunukuu baadhi ya semi ambazo zinasemekana zinatumiwa na wazazi katika shughuli ya kulea watoto.
Ni kweli kwamba lugha yoyote ile hufanya kazi nyingi sana kama vile kutumbuiza watu, kuficha siri, kuseng’enya watu, kuibia watu, kutongozana, kushawishi, kugombana, kujitetea, kufundisha, nakadhalika.
Hii ni kwa sababu bila kutumia lugha, mtu hawezi akaimba, akagombana, akaiba kwa kudang’anya, akafundisha, akaseng’enya, akatongoza, n.
k.
Hata hivyo, katika makala haya, mtafiti alijikita kwenye malezi ya watoto.
Katika kazi hii, mtafiti alizingatia semi mbalimbali ambazo Wamasaaba huzitumia kwa ajili ya kuwaelekeza watoto wao ili wasije wakatenda maovu ukubwani.
Katika jamii mbalimbali, watu hutumia lugha kutekeleza jambo hili.
Jamii hasa zile za jadi zilitumia lugha kuwaelekeza watoto wao.
Kuna namna ambavyo walisuka lugha kisanaa kwa lengo la kufunza watoto wao.
Hii ni kwa sababu hawakuwa na madarasa maalumu mwa kufunzia watoto wao kama ilivyo sasa.
Katika jamii hizo, shule zenyewe hazikuwepo.
Kwa hiyo, lugha ndiyo ilikuwa chombo maalumu cha kufunzia watoto.
Matumizi ya lugha yalidhamiria kukuza watoto wenye tabia nzuri.
Hii ni kwa sababu watoto wenye tabia mbaya waliletea wazazi wao aibu.
Hivyo basi, katika kazi hii, mtafiti alijikita katika matumizi ya lugha na kueleza jinsi Wamasaaba wanavyotumia semi mbalimbali kuelekeza watoto wao kitabia.

Related Results

Uraia, Lugha na Haki za Kidijitali: umuhimu wa lugha katika harakati za kuondoa ukoloni katika teknolojia
Uraia, Lugha na Haki za Kidijitali: umuhimu wa lugha katika harakati za kuondoa ukoloni katika teknolojia
Purpose Maneno mengi yanayohusu haki za binadamu na haki za kiteknolojia hayajatafsiriwa katika lugha ya Kiswahili. Kwa hivyo, wataalamu wa teknolojia na watetezi wa haki za kidiji...
Uamilifu wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Kimatumizi kwenye Kaunti ya Bungoma
Uamilifu wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Kimatumizi kwenye Kaunti ya Bungoma
Lugha ni chombo maalum katika ustawishaji na uimarishaji wa rasilimali za mwanadamu. Pia, ni wenzo unaohimili sera ambazo hulenga katika kutimiza matarajio ya kitaifa katika nchi y...
Matumizi ya Kiswahili katika Ujumuishaji wa Kidemokrasia kwenye Uchaguzi Nchini Tanzania
Matumizi ya Kiswahili katika Ujumuishaji wa Kidemokrasia kwenye Uchaguzi Nchini Tanzania
Makala haya yanaeleza matumizi ya lugha ya Kiswahili katika ujumuishaji wa kidemokrasia nchini Tanzania kwa kuzingatia matumizi ya lugha hiyo kwenye michakato ya uchaguzi. Lengo la...
Athari za Usasa kwenye Usimulizi wa Hadithi katika Jamii ya Wamasaaba Nchini Uganda
Athari za Usasa kwenye Usimulizi wa Hadithi katika Jamii ya Wamasaaba Nchini Uganda
Katika makala haya, watafiti anaeleza jinsi usimulizi wa hadithi umeathiriwa na usasa katika jamii ya Wamasaaba nchini Uganda. Anafanya hivyo kwa kulinganisha hali ilivyo sasa na j...
Nafasi ya Ikolojia ya Lugha katika Mtagusano wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Dini katika Kaunti ya Bungoma
Nafasi ya Ikolojia ya Lugha katika Mtagusano wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Dini katika Kaunti ya Bungoma
Nyanja mbalimbali katika jamii hutegemea matumizi ya lugha. Hali hii huzua changamoto ya namna ya kutumia raslimali za lugha zinazopatikana katika jamiilugha fulani. Juhudi ya kufa...
Matumizi ya Kiswahili katika Mawasiliano na Uongozi wa Kidini katika Shule za Upili Nchini Kenya: Mfano wa Shule ya Wasichana ya Itigo
Matumizi ya Kiswahili katika Mawasiliano na Uongozi wa Kidini katika Shule za Upili Nchini Kenya: Mfano wa Shule ya Wasichana ya Itigo
Utafiti huu ulichunguza matumizi ya Kiswahili katika mawasiliano na uongozi wa kidini katika shule ya wasichana ya Itigo. Ulilenga kubaini jinsi lugha ya Kiswahili hutumika katika ...
Vipengele Vya Fasihi Vinavyojenga Taswira Ya Mwanamke Katikavitabu Teule Vya Biblia Takatifu
Vipengele Vya Fasihi Vinavyojenga Taswira Ya Mwanamke Katikavitabu Teule Vya Biblia Takatifu
Lugha ni chombo cha kipekee kinachofinyangwa kuwasilisha taswira ya masuala changamano katika jamii. Matokeo haya ya lugha ni fasihi, ambayo ni kioo cha jamii. Biblia Takatifu ni k...
Mnyambuliko wa Vitenzi Katika Lugha za Kiafrika: Mfano katika Lugha ya Kimasaaba Nchini Uganda
Mnyambuliko wa Vitenzi Katika Lugha za Kiafrika: Mfano katika Lugha ya Kimasaaba Nchini Uganda
Katika makala hii, mtafiti anaeleza jinsi vitenzi vya lugha za Kiafrika vinavyonyambuliwa na kuleta maana tofauti tofauti. Anafanya hivyo kwa kurejelea Kimasaaba ambayo ni lugha in...

Back to Top