Search engine for discovering works of Art, research articles, and books related to Art and Culture
ShareThis
Javascript must be enabled to continue!

Mikakati ya Upole Katika Mawasiliano ya Wahudumu wa Magari ya Uchukuzi na Abiria katika lugha ya Kikamba.

View through CrossRef
Upole ni hali ya msemaji kudhihirisha kuwa anajali hisia na mahitaji ya msikilizaji katika mazungumzo. Mikakati ya upole hutumiwa na washiriki wa mazungumzo kulainisha na kufanikisha mazungumzo yao. Makala hii inachanganua mikakati ya upole inayotumiwa na wahudumu wa magari ya uchukuzi wa umma wanapoingiliana na abiria katika mji wa Matuu kwa kuzingatia lugha ya Kikamba. Mji wa Matuu upo katika kaunti ya Machakos, kaunti ndogo ya Yatta. Sampuli ya utafiti huu ilichaguliwa kimakusudi. Data ya utafiti huu ilikusanywa katika vituo vitatu vya magari ya uchukuzi katika mji wa Matuu vilivyoteuliwa kimakusudi. Mtafiti aliwahoji wahudumu ishirini na wawili na abiria kumi na tano. Mazungumzo kati ya wahudumu wa magari na abiria yalirekodiwa kwa kutumia kinasa sauti. Njia ya uchunguzi ilitumika kuchunguza mbinu ishara za kuwasiliana kama vile ishara za uso. Kauli zilizo na mikakati ya upole zilinakiliwa na kuwekwa kwenye makundi matano ya mikakati ya upole ili kuchanganuliwa. Makundi hayo ni: Mkakati wa kuwa kwenye rekodi, mkakati chanya wa upole, mkakati hasi wa upole, mkakati wa kuwa nje ya rekodi na mkakati wa kutosema chochote. Utafiti huu uliongozwa na mihimili ya Nadharia ya Upole ya Brown na Levinson (1978, 1987). Matokeo ya utafiti huu yameonyesha kuwa wahudumu walitumia mikakati yote tano ya upole ili kulainisha mawasiliano kati yao na abiria. Mkakati chanya wa upole na mkakati hasi wa upole ndiyo iliyotumika kwa wingi na katika vituo vyote vitatu. Kupitia utafiti huu mtafiti anaamini kuwa washikadau katika sekta ya uchukuzi watapata maarifa kuhusu mbinu za kuwasiliana na abiria ili kutimiza malengo yao. Vile vile, kazi hii itasaidia kuboresha matumizi ya lugha kati ya wanajamii pamoja na kuongezea maarifa yaliyomo kuhusiana na taaluma ya isimujamii.
Title: Mikakati ya Upole Katika Mawasiliano ya Wahudumu wa Magari ya Uchukuzi na Abiria katika lugha ya Kikamba.
Description:
Upole ni hali ya msemaji kudhihirisha kuwa anajali hisia na mahitaji ya msikilizaji katika mazungumzo.
Mikakati ya upole hutumiwa na washiriki wa mazungumzo kulainisha na kufanikisha mazungumzo yao.
Makala hii inachanganua mikakati ya upole inayotumiwa na wahudumu wa magari ya uchukuzi wa umma wanapoingiliana na abiria katika mji wa Matuu kwa kuzingatia lugha ya Kikamba.
Mji wa Matuu upo katika kaunti ya Machakos, kaunti ndogo ya Yatta.
Sampuli ya utafiti huu ilichaguliwa kimakusudi.
Data ya utafiti huu ilikusanywa katika vituo vitatu vya magari ya uchukuzi katika mji wa Matuu vilivyoteuliwa kimakusudi.
Mtafiti aliwahoji wahudumu ishirini na wawili na abiria kumi na tano.
Mazungumzo kati ya wahudumu wa magari na abiria yalirekodiwa kwa kutumia kinasa sauti.
Njia ya uchunguzi ilitumika kuchunguza mbinu ishara za kuwasiliana kama vile ishara za uso.
Kauli zilizo na mikakati ya upole zilinakiliwa na kuwekwa kwenye makundi matano ya mikakati ya upole ili kuchanganuliwa.
Makundi hayo ni: Mkakati wa kuwa kwenye rekodi, mkakati chanya wa upole, mkakati hasi wa upole, mkakati wa kuwa nje ya rekodi na mkakati wa kutosema chochote.
Utafiti huu uliongozwa na mihimili ya Nadharia ya Upole ya Brown na Levinson (1978, 1987).
Matokeo ya utafiti huu yameonyesha kuwa wahudumu walitumia mikakati yote tano ya upole ili kulainisha mawasiliano kati yao na abiria.
Mkakati chanya wa upole na mkakati hasi wa upole ndiyo iliyotumika kwa wingi na katika vituo vyote vitatu.
Kupitia utafiti huu mtafiti anaamini kuwa washikadau katika sekta ya uchukuzi watapata maarifa kuhusu mbinu za kuwasiliana na abiria ili kutimiza malengo yao.
Vile vile, kazi hii itasaidia kuboresha matumizi ya lugha kati ya wanajamii pamoja na kuongezea maarifa yaliyomo kuhusiana na taaluma ya isimujamii.

Related Results

Mchango wa Mikakati ya Upole Katika Mazungumzo ya ibada ya Mazishi katika Lugha ya Kikabrasi
Mchango wa Mikakati ya Upole Katika Mazungumzo ya ibada ya Mazishi katika Lugha ya Kikabrasi
Swahili Suala la upole limetafitiwa na wasomi wengi kwenye mawasiliano, ikiwemo mazungumzo ya abiria na wahudumu wa magari ya uchukuzi kwa lugha ya Kikamba. Hata hivyo, utafiti huu...
Upole katika Manifesto ya Kenya Kwanza
Upole katika Manifesto ya Kenya Kwanza
Upole ni suala ambalo limeshughulikiwa na wanazuoni mbalimbali katika tamthilia, vipindi vya runinga, mawasiliano ya bodaboda na abiria na mazungumzo ya redioni. Makala hii inadham...
Uraia, Lugha na Haki za Kidijitali: umuhimu wa lugha katika harakati za kuondoa ukoloni katika teknolojia
Uraia, Lugha na Haki za Kidijitali: umuhimu wa lugha katika harakati za kuondoa ukoloni katika teknolojia
Purpose Maneno mengi yanayohusu haki za binadamu na haki za kiteknolojia hayajatafsiriwa katika lugha ya Kiswahili. Kwa hivyo, wataalamu wa teknolojia na watetezi wa haki za kidiji...
Uamilifu wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Kimatumizi kwenye Kaunti ya Bungoma
Uamilifu wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Kimatumizi kwenye Kaunti ya Bungoma
Lugha ni chombo maalum katika ustawishaji na uimarishaji wa rasilimali za mwanadamu. Pia, ni wenzo unaohimili sera ambazo hulenga katika kutimiza matarajio ya kitaifa katika nchi y...
Matumizi ya Kiswahili katika Mawasiliano na Uongozi wa Kidini katika Shule za Upili Nchini Kenya: Mfano wa Shule ya Wasichana ya Itigo
Matumizi ya Kiswahili katika Mawasiliano na Uongozi wa Kidini katika Shule za Upili Nchini Kenya: Mfano wa Shule ya Wasichana ya Itigo
Utafiti huu ulichunguza matumizi ya Kiswahili katika mawasiliano na uongozi wa kidini katika shule ya wasichana ya Itigo. Ulilenga kubaini jinsi lugha ya Kiswahili hutumika katika ...
Nafasi ya Ikolojia ya Lugha katika Mtagusano wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Dini katika Kaunti ya Bungoma
Nafasi ya Ikolojia ya Lugha katika Mtagusano wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Dini katika Kaunti ya Bungoma
Nyanja mbalimbali katika jamii hutegemea matumizi ya lugha. Hali hii huzua changamoto ya namna ya kutumia raslimali za lugha zinazopatikana katika jamiilugha fulani. Juhudi ya kufa...
Vipengele Vya Fasihi Vinavyojenga Taswira Ya Mwanamke Katikavitabu Teule Vya Biblia Takatifu
Vipengele Vya Fasihi Vinavyojenga Taswira Ya Mwanamke Katikavitabu Teule Vya Biblia Takatifu
Lugha ni chombo cha kipekee kinachofinyangwa kuwasilisha taswira ya masuala changamano katika jamii. Matokeo haya ya lugha ni fasihi, ambayo ni kioo cha jamii. Biblia Takatifu ni k...
Kuwezeshwa kwa uchumi kupitia lugha ya kiswahili
Kuwezeshwa kwa uchumi kupitia lugha ya kiswahili
Makala haya yanalenga kuangazia juhudi za nchi za Afrika mashariki na bara la Afrika kutumia Kiswahili kama nyenzo ya mawasiliono miongoni mwao ili kurahisisha mawasiliano na biash...

Back to Top