Search engine for discovering works of Art, research articles, and books related to Art and Culture
ShareThis
Javascript must be enabled to continue!

Mustakabali wa Kiswahili kama Lugha ya Kufundishia Nchini Tanzania: Uhakiki wa Maudhui ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya 2014

View through CrossRef
Msingi wa makala haya ni “Sera ya Elimu na Mafunzo” (SEM, 2014). Makala yanahakiki nafasi ya lugha ya Kiswahili kwenye Sera ya Elimu na Mafunzo nchini Tanzania na mustakabali wake kwenye mfumo wa elimu kama lugha ya kufundishia. Mbinu iliyotumika ni ya maktabani ambapo mwandishi alisoma na kuhakiki maudhui ya SEM msisitizo ukiwa kwenye masuala yahusuyo lugha ya kufundishia. Uchambuzi wa kiisimujamii ulitumika ili kuonesha ukinzani baina ya matamko ya SEM. Tamko la SEM kuhusu lugha ya Kiswahili kama lugha ya kufundishia haliakisi hali halisi. Uhusiano wa Kiisimujamii wa lugha ya Kiswahili na ya Kiingereza kuhusu elimu unatoa tafsiri kuwa endapo SEM itatumika bila nia ya dhati ya kuisaidia lugha ya Kiswahili basi lugha hiyo inaweza kutoweka kabisa kwenye mfumo wa elimu kama lugha ya kufundishia. Makala yanajenga hoja kuwa tamko la SEM kwamba Kiingereza na Kiswahili ziwe na hadhi sawa kwenye mfumo wa elimu linatia moyo kwa mustakabali wa lugha ya Kiswahili lakini utekelezaji wake unaibua changamoto nyingi kwa namna ambayo zisipotazamwa kwa makini lugha ya Kiingereza itaendelea kukita mizizi zaidi na kujenga uwezekano wa jamii kukataa kufundishwa kwa lugha ya Kiswahili kwa sababu mwelekeo wa jamii unanasibisha elimu na Kiingereza. Mwisho, wito unatolewa kwa watunga sera kusitisha kutumia lugha ya wachache kutoa elimu kwa wengi kwa kuwa kufanya hivyo ni kubadili malengo ya elimu.
Mkwawa University College of Education
Title: Mustakabali wa Kiswahili kama Lugha ya Kufundishia Nchini Tanzania: Uhakiki wa Maudhui ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya 2014
Description:
Msingi wa makala haya ni “Sera ya Elimu na Mafunzo” (SEM, 2014).
Makala yanahakiki nafasi ya lugha ya Kiswahili kwenye Sera ya Elimu na Mafunzo nchini Tanzania na mustakabali wake kwenye mfumo wa elimu kama lugha ya kufundishia.
Mbinu iliyotumika ni ya maktabani ambapo mwandishi alisoma na kuhakiki maudhui ya SEM msisitizo ukiwa kwenye masuala yahusuyo lugha ya kufundishia.
Uchambuzi wa kiisimujamii ulitumika ili kuonesha ukinzani baina ya matamko ya SEM.
Tamko la SEM kuhusu lugha ya Kiswahili kama lugha ya kufundishia haliakisi hali halisi.
Uhusiano wa Kiisimujamii wa lugha ya Kiswahili na ya Kiingereza kuhusu elimu unatoa tafsiri kuwa endapo SEM itatumika bila nia ya dhati ya kuisaidia lugha ya Kiswahili basi lugha hiyo inaweza kutoweka kabisa kwenye mfumo wa elimu kama lugha ya kufundishia.
Makala yanajenga hoja kuwa tamko la SEM kwamba Kiingereza na Kiswahili ziwe na hadhi sawa kwenye mfumo wa elimu linatia moyo kwa mustakabali wa lugha ya Kiswahili lakini utekelezaji wake unaibua changamoto nyingi kwa namna ambayo zisipotazamwa kwa makini lugha ya Kiingereza itaendelea kukita mizizi zaidi na kujenga uwezekano wa jamii kukataa kufundishwa kwa lugha ya Kiswahili kwa sababu mwelekeo wa jamii unanasibisha elimu na Kiingereza.
Mwisho, wito unatolewa kwa watunga sera kusitisha kutumia lugha ya wachache kutoa elimu kwa wengi kwa kuwa kufanya hivyo ni kubadili malengo ya elimu.

Related Results

Uraia, Lugha na Haki za Kidijitali: umuhimu wa lugha katika harakati za kuondoa ukoloni katika teknolojia
Uraia, Lugha na Haki za Kidijitali: umuhimu wa lugha katika harakati za kuondoa ukoloni katika teknolojia
Purpose Maneno mengi yanayohusu haki za binadamu na haki za kiteknolojia hayajatafsiriwa katika lugha ya Kiswahili. Kwa hivyo, wataalamu wa teknolojia na watetezi wa haki za kidiji...
Mabadiliko katika Mtaala wa Elimu ya Msingi na Namna Yanavyoathiri Tathmini katika Elimu ya Juu
Mabadiliko katika Mtaala wa Elimu ya Msingi na Namna Yanavyoathiri Tathmini katika Elimu ya Juu
Makala haya yamekusudia kuchunguza namna ambavyo mabadiliko katika mtaala wa elimu ya msingi yanavyoathiri tathmini katika elimu ya juu. Mabadiliko ya mtaala yanafanyika katika nga...
Visababishi vya Idadi Kubwa ya Wanafunzi wa Shule za Sekondari Nchini Uganda Kutochukua Somo la Kiswahili
Visababishi vya Idadi Kubwa ya Wanafunzi wa Shule za Sekondari Nchini Uganda Kutochukua Somo la Kiswahili
Katika makala haya, mtafiti anaeleza visababishi vya idadi kubwa ya wanafunzi katika shule za upili nchini Uganda kutochukua somo la Kiswahili. Wakati wa kupunguza idadi ya masomo ...
Maoni ya wanafunzi wa taasisi za kiufundi za kitaifa kuhusu nafasi ya Kiswahili katika elimu ya ufundi nchini Kenya
Maoni ya wanafunzi wa taasisi za kiufundi za kitaifa kuhusu nafasi ya Kiswahili katika elimu ya ufundi nchini Kenya
Utafiti huu ulinuia kutafuta maoni ya wanafunzi wa taasisi za kiufundi za kitaifa kuhusu nafasi ya lugha ya Kiswahili katika elimu ya kiufundi. Muundo wa Uchunguzi Kimaelezo ulitum...
Matumizi ya Kiswahili katika Ujumuishaji wa Kidemokrasia kwenye Uchaguzi Nchini Tanzania
Matumizi ya Kiswahili katika Ujumuishaji wa Kidemokrasia kwenye Uchaguzi Nchini Tanzania
Makala haya yanaeleza matumizi ya lugha ya Kiswahili katika ujumuishaji wa kidemokrasia nchini Tanzania kwa kuzingatia matumizi ya lugha hiyo kwenye michakato ya uchaguzi. Lengo la...
Uamilifu wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Kimatumizi kwenye Kaunti ya Bungoma
Uamilifu wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Kimatumizi kwenye Kaunti ya Bungoma
Lugha ni chombo maalum katika ustawishaji na uimarishaji wa rasilimali za mwanadamu. Pia, ni wenzo unaohimili sera ambazo hulenga katika kutimiza matarajio ya kitaifa katika nchi y...
Matumizi ya Kiswahili katika Mawasiliano na Uongozi wa Kidini katika Shule za Upili Nchini Kenya: Mfano wa Shule ya Wasichana ya Itigo
Matumizi ya Kiswahili katika Mawasiliano na Uongozi wa Kidini katika Shule za Upili Nchini Kenya: Mfano wa Shule ya Wasichana ya Itigo
Utafiti huu ulichunguza matumizi ya Kiswahili katika mawasiliano na uongozi wa kidini katika shule ya wasichana ya Itigo. Ulilenga kubaini jinsi lugha ya Kiswahili hutumika katika ...
Kuchambua Athari ya Vivumishi vya Runyakitara Katika Ujifunzaji wa Lugha ya Kiswahili Nchini Uganda
Kuchambua Athari ya Vivumishi vya Runyakitara Katika Ujifunzaji wa Lugha ya Kiswahili Nchini Uganda
Katika mfumo wa elimu nchini Uganda, Kiswahili ni lugha muhimu kwa mawasiliano na maendeleo ya kijamii. Hata hivyo, wanafunzi wanaozungumza Runyakitara wanakumbana na changamoto ka...

Back to Top