Javascript must be enabled to continue!
Sitiari Dhanifu Katika Mazungumzo ya Hafla ya Mahari Katika Jamii ya Agikuyu
View through CrossRef
Utafiti huu ulizitathmini sitiari dhanifu ambazo huibuka katika mchakato ufungamanishwao na hafla za majadiliano ya mahari katika awamu mbalimbali za shughuli hiyo muhimu katika jamii ya Agikuyu inayorejelewa kama “Ruracio”. Matumizi ya sitiari katika kujenga majadiliano huwa uti wa mgongo na kwa sababu hiyo wawakilishi wanaoteuliwa na pande mbili za aila husika huhitajiwa kuwa na umilisi mpevu wa lugha husika ili kufaulisha shughuli hiyo. Ikumbukwe kuwa, sitiari zinazotumiwa katika mchakato husika huchangia kujenga ukuruba baina ya koo husika kwa mujibu wa mila na desturi za jamii ya Agikuyu popote pale inapojikuta. Data iliyokusanywa ilirekodiwa kutoka mazungumzo halisi ya hafla husika ambapo mtafiti alivihudhuria vikao vitano tofauti lengo likiwa kuipata data ambayo kwa mujibu wa utafiti ingesemwa kuwa tegemevu. Kama mshiriki, mtafiti alizihudhuria hafla mbili katika gatuzi la Muranga na tatu katika gatuzi la Nakuru anakokaa. Data ilitafsiriwa na kuainishwa kwa mujibu wa maratokezi na hatimaye kuelezewa. Sitiari nyingi zilizojitokeza zilifungamana na vitambulisho vya kijinsia. Aidha, sitiari hizo zikijikita katika matukio tofauti tofauti ya mchakato wote wa sherehe hiyo. Ilibainika kuwa, sitiari husheheni hafla hii kwa kiwango kikubwa zikichangia kuingiliana na kukamilisha awamu tofauti tofauti za mitagusano ya jamii hii ya Agikuyu. Matokeo ya utafiti huu bila shaka yatajenga dafina bora ya wasomi katika uwanja wa fasihi na uchanganuzi lugha
East African Nature and Science Organization
Title: Sitiari Dhanifu Katika Mazungumzo ya Hafla ya Mahari Katika Jamii ya Agikuyu
Description:
Utafiti huu ulizitathmini sitiari dhanifu ambazo huibuka katika mchakato ufungamanishwao na hafla za majadiliano ya mahari katika awamu mbalimbali za shughuli hiyo muhimu katika jamii ya Agikuyu inayorejelewa kama “Ruracio”.
Matumizi ya sitiari katika kujenga majadiliano huwa uti wa mgongo na kwa sababu hiyo wawakilishi wanaoteuliwa na pande mbili za aila husika huhitajiwa kuwa na umilisi mpevu wa lugha husika ili kufaulisha shughuli hiyo.
Ikumbukwe kuwa, sitiari zinazotumiwa katika mchakato husika huchangia kujenga ukuruba baina ya koo husika kwa mujibu wa mila na desturi za jamii ya Agikuyu popote pale inapojikuta.
Data iliyokusanywa ilirekodiwa kutoka mazungumzo halisi ya hafla husika ambapo mtafiti alivihudhuria vikao vitano tofauti lengo likiwa kuipata data ambayo kwa mujibu wa utafiti ingesemwa kuwa tegemevu.
Kama mshiriki, mtafiti alizihudhuria hafla mbili katika gatuzi la Muranga na tatu katika gatuzi la Nakuru anakokaa.
Data ilitafsiriwa na kuainishwa kwa mujibu wa maratokezi na hatimaye kuelezewa.
Sitiari nyingi zilizojitokeza zilifungamana na vitambulisho vya kijinsia.
Aidha, sitiari hizo zikijikita katika matukio tofauti tofauti ya mchakato wote wa sherehe hiyo.
Ilibainika kuwa, sitiari husheheni hafla hii kwa kiwango kikubwa zikichangia kuingiliana na kukamilisha awamu tofauti tofauti za mitagusano ya jamii hii ya Agikuyu.
Matokeo ya utafiti huu bila shaka yatajenga dafina bora ya wasomi katika uwanja wa fasihi na uchanganuzi lugha.
Related Results
Mabadiliko katika Mtaala wa Elimu ya Msingi na Namna Yanavyoathiri Tathmini katika Elimu ya Juu
Mabadiliko katika Mtaala wa Elimu ya Msingi na Namna Yanavyoathiri Tathmini katika Elimu ya Juu
Makala haya yamekusudia kuchunguza namna ambavyo mabadiliko katika mtaala wa elimu ya msingi yanavyoathiri tathmini katika elimu ya juu. Mabadiliko ya mtaala yanafanyika katika nga...
Ubainishaji wa Vipengele vya Ujumi wa Kiafrika na Athari yake katika Ushairi wa Kiswahili: Uchunguzi wa Ushairi wa Bongo Fleva
Ubainishaji wa Vipengele vya Ujumi wa Kiafrika na Athari yake katika Ushairi wa Kiswahili: Uchunguzi wa Ushairi wa Bongo Fleva
Makala haya yalichunguza ujitokezaji wa ujumi wa Kiafrika katika ushairi wa Kiswahili wa Bongo Fleva pamoja na athari yake katika ushairi huo. Tafiti kuhusu vipengele vya ujumi wa ...
Jinsi Masuala ya Kijinsia Yalivyo Shughulikiwa Katika Tamthilia ya ‘Bembea ya Maisha’ kwa Kuzingatia Jinsia ya Mwandishi
Jinsi Masuala ya Kijinsia Yalivyo Shughulikiwa Katika Tamthilia ya ‘Bembea ya Maisha’ kwa Kuzingatia Jinsia ya Mwandishi
Maumbile ya binadamu yamechukua mikondo miwili; mwanamume na mwanamke. Jamii tofauti hutoa majukumu kwa kuzingatia migao hii miwili. Hivi ni kusema kuwa, shughuli za mtu katika jam...
Uraia, Lugha na Haki za Kidijitali: umuhimu wa lugha katika harakati za kuondoa ukoloni katika teknolojia
Uraia, Lugha na Haki za Kidijitali: umuhimu wa lugha katika harakati za kuondoa ukoloni katika teknolojia
Purpose
Maneno mengi yanayohusu haki za binadamu na haki za kiteknolojia hayajatafsiriwa katika lugha ya Kiswahili. Kwa hivyo, wataalamu wa teknolojia na watetezi wa haki za kidiji...
Nafasi ya Ikolojia ya Lugha katika Mtagusano wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Dini katika Kaunti ya Bungoma
Nafasi ya Ikolojia ya Lugha katika Mtagusano wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Dini katika Kaunti ya Bungoma
Nyanja mbalimbali katika jamii hutegemea matumizi ya lugha. Hali hii huzua changamoto ya namna ya kutumia raslimali za lugha zinazopatikana katika jamiilugha fulani. Juhudi ya kufa...
Matumizi ya Lugha Kwenye Malezi ya Watoto: Mfano wa Matumizi ya Semi Katika Jamii ya Wamasaaba Nchini Uganda
Matumizi ya Lugha Kwenye Malezi ya Watoto: Mfano wa Matumizi ya Semi Katika Jamii ya Wamasaaba Nchini Uganda
Katika makala haya, mtafiti anaeleza jinsi lugha inavyotumiwa na wazazi katika shughuli yao ya kulea watoto. Alifanya hivyo kwa kurejelea malezi ya watoto katika jamii ya Wamasaaba...
Mchango wa Mikakati ya Upole Katika Mazungumzo ya ibada ya Mazishi katika Lugha ya Kikabrasi
Mchango wa Mikakati ya Upole Katika Mazungumzo ya ibada ya Mazishi katika Lugha ya Kikabrasi
Swahili
Suala la upole limetafitiwa na wasomi wengi kwenye mawasiliano, ikiwemo mazungumzo ya abiria na wahudumu wa magari ya uchukuzi kwa lugha ya Kikamba. Hata hivyo, utafiti huu...
Ujitokezaji wa Viarudhi vya Kifonolojia katika Kihaya: Uchunguzi Kifani wa Toni katika Lahaja ya Kihamba
Ujitokezaji wa Viarudhi vya Kifonolojia katika Kihaya: Uchunguzi Kifani wa Toni katika Lahaja ya Kihamba
Fonolojia ni taaluma iliyosheheni viarudhi au vipambasauti kama ambavyo wataalamu wengine huviita. Miongoni mwake ni toni, lafudhi, mkazo, nguvumsikiko, usilabi, kiimbo, unguvunguv...

