Search engine for discovering works of Art, research articles, and books related to Art and Culture
ShareThis
Javascript must be enabled to continue!

Utabirifu wa Makosa ya Utenganishaji na Uunganishaji wa Maneno katika Kiswahili

View through CrossRef
Uandishi ni mchakato unaohitaji umakini ili kinachoandikwa kieleweke kwa msomaji kwa namna iliyokusudiwa na mwandishi. Ikiwa kueleweka kutazingatiwa, basi, kutakuwa na mawasiliano madhubuti. Hata hivyo, matini mbalimbali zimekuwa na makosa mengi kiasi cha kukwamisha mawasiliano baina ya mwandishi na msomaji wake. Lengo la makala haya ni kuchunguza utabirifu wa makosa katika uandishi kwa kumakinikia makosa ya utenganishaji na uunganishaji wa maneno. Nadharia ya Uchanganuzi Makosa ya Corder (1967) imetumika kuchambua na kujadili data za utafiti kwa sababu inahusika na makosa yanayohusiana na lugha na isimu. Data zimekusanywa kwa kutumia mbinu ya uchambuzi wa matini na usaili. Matokeo ya utafiti yanaonesha kwamba makosa ya kutenganisha na kuunganisha maneno yanatabirika kwa sababu yana uelekeo mmoja. Makosa ya kuunganisha maneno yamegawanyika katika makundi makubwa manne, yaani maneno yenye urejeshi, maneno yenye kiambishi cha umahali na wakati, maneno yanayotokana na uradidi, na maneno ambatani. Makosa ya kuunganisha maneno yamegawanyika katika makundi mawili ambayo ni mwambatano wa vitenzi shirikishi vya “kuwa na” na nomino, na viunganishi tegemezi vinavyoanza na “kwa”. Kwa ujumla, makosa haya yanatokana na uhamishaji wa kanuni moja katika uandishi wa maneno fulani yenye vipashio, hususani viambishi vinavyofanana. Kufuatia matokeo haya, makala haya yanapendekeza waandishi kuzingatia aina na sifa mahususi za maneno na si kujumuisha kanuni zinazotumika kuandika baadhi ya maneno.
University of Dar es Salaam
Title: Utabirifu wa Makosa ya Utenganishaji na Uunganishaji wa Maneno katika Kiswahili
Description:
Uandishi ni mchakato unaohitaji umakini ili kinachoandikwa kieleweke kwa msomaji kwa namna iliyokusudiwa na mwandishi.
Ikiwa kueleweka kutazingatiwa, basi, kutakuwa na mawasiliano madhubuti.
Hata hivyo, matini mbalimbali zimekuwa na makosa mengi kiasi cha kukwamisha mawasiliano baina ya mwandishi na msomaji wake.
Lengo la makala haya ni kuchunguza utabirifu wa makosa katika uandishi kwa kumakinikia makosa ya utenganishaji na uunganishaji wa maneno.
Nadharia ya Uchanganuzi Makosa ya Corder (1967) imetumika kuchambua na kujadili data za utafiti kwa sababu inahusika na makosa yanayohusiana na lugha na isimu.
Data zimekusanywa kwa kutumia mbinu ya uchambuzi wa matini na usaili.
Matokeo ya utafiti yanaonesha kwamba makosa ya kutenganisha na kuunganisha maneno yanatabirika kwa sababu yana uelekeo mmoja.
Makosa ya kuunganisha maneno yamegawanyika katika makundi makubwa manne, yaani maneno yenye urejeshi, maneno yenye kiambishi cha umahali na wakati, maneno yanayotokana na uradidi, na maneno ambatani.
Makosa ya kuunganisha maneno yamegawanyika katika makundi mawili ambayo ni mwambatano wa vitenzi shirikishi vya “kuwa na” na nomino, na viunganishi tegemezi vinavyoanza na “kwa”.
Kwa ujumla, makosa haya yanatokana na uhamishaji wa kanuni moja katika uandishi wa maneno fulani yenye vipashio, hususani viambishi vinavyofanana.
Kufuatia matokeo haya, makala haya yanapendekeza waandishi kuzingatia aina na sifa mahususi za maneno na si kujumuisha kanuni zinazotumika kuandika baadhi ya maneno.

Related Results

Ushairi WA Kiganda Unavyoweza Kuchangia Na Kuendeleza Ushairi WA Kiswahili Kimtindo Na Kimaudhui: Mfano WA Ufundishaji Nchini Uganda
Ushairi WA Kiganda Unavyoweza Kuchangia Na Kuendeleza Ushairi WA Kiswahili Kimtindo Na Kimaudhui: Mfano WA Ufundishaji Nchini Uganda
Wanafunzi wengi nchini Uganda wanachukulia utanzu wa ushairi wa Kiswahili kuwa mgumu na wanapata ugumu katika kujifunza ushairi wa Kiswahili. Ushairi wa Kiganda umekuwa unatendwa v...
Mabadiliko katika Mtaala wa Elimu ya Msingi na Namna Yanavyoathiri Tathmini katika Elimu ya Juu
Mabadiliko katika Mtaala wa Elimu ya Msingi na Namna Yanavyoathiri Tathmini katika Elimu ya Juu
Makala haya yamekusudia kuchunguza namna ambavyo mabadiliko katika mtaala wa elimu ya msingi yanavyoathiri tathmini katika elimu ya juu. Mabadiliko ya mtaala yanafanyika katika nga...
Muundo wa Kifonolojia wa Maneno ya Sheng’
Muundo wa Kifonolojia wa Maneno ya Sheng’
Utafiti huu ulidhamiria kutathmini athari za kamusi ya Sheng’ – English Dictionary kwa Kiswahili sanifu. Kamusi ya Sheng’ – English Dictionary (2003) iliteuliwa kama msingi wa uchu...
Uambikaji wa Viambishi Ngeli katika Nomino Sahili Zinazorejelea Ndugu na Maana yake katika Sarufi ya Kiswahili
Uambikaji wa Viambishi Ngeli katika Nomino Sahili Zinazorejelea Ndugu na Maana yake katika Sarufi ya Kiswahili
Nomino sahili ni maneno ambayo kimofolojia yameundwa na mofu huru moja. Pia, kisematiki, maneno haya yana maana zake katika kamusi. Licha ya kuwa na sifa hizi, uambikaji wa viambis...
Kubainisha Kanuni na Sheria Zinazotawala Muundo wa Maneno katika Sentensi Sahili ya Ekegusii.
Kubainisha Kanuni na Sheria Zinazotawala Muundo wa Maneno katika Sentensi Sahili ya Ekegusii.
Utafiti huu unalenga kubainisha kanuni na sheria zinazotawala muundo wa maneno katika sentensi sahili ya Ekegusii. Utafiti huu ulihasisiwa na nadharia ya Sintaksia Finyizi. Utafiti...
Athari za Mtaala wa Umilisi katika Ukuzaji wa Umahiri wa Kuzungumza Kiswahili kwa Wanafunzi wa Shule za Sekondari Nchini Uganda
Athari za Mtaala wa Umilisi katika Ukuzaji wa Umahiri wa Kuzungumza Kiswahili kwa Wanafunzi wa Shule za Sekondari Nchini Uganda
Umahiri wa kuzungumza lugha ni miongoni mwa matokeo yanayotarajiwa kutoka kwa mtu yeyote anayejifunza lugha ya kigeni au lugha ya pili. Mathalani nchini Uganda imebainika kuwa kiwa...
Jinsi Masuala ya Kijinsia Yalivyo Shughulikiwa Katika Tamthilia ya ‘Bembea ya Maisha’ kwa Kuzingatia Jinsia ya Mwandishi
Jinsi Masuala ya Kijinsia Yalivyo Shughulikiwa Katika Tamthilia ya ‘Bembea ya Maisha’ kwa Kuzingatia Jinsia ya Mwandishi
Maumbile ya binadamu yamechukua mikondo miwili; mwanamume na mwanamke. Jamii tofauti hutoa majukumu kwa kuzingatia migao hii miwili. Hivi ni kusema kuwa, shughuli za mtu katika jam...
Ulinganishi Wa Uundaji Wa Maneno Ya Kiswahili Na Ya Kiarabu
Ulinganishi Wa Uundaji Wa Maneno Ya Kiswahili Na Ya Kiarabu
Makala hii imejadili suala la ulinganishi wa uundaji wa maneno ya Kiswahili na Kiarabu. Katika makala hii tumetoa taarifa kuhusu umuhimu na njia za uundaji wa maneno kwa jumla, aid...

Back to Top