Search engine for discovering works of Art, research articles, and books related to Art and Culture
ShareThis
Javascript must be enabled to continue!

Uambikaji wa Viambishi Ngeli katika Nomino Sahili Zinazorejelea Ndugu na Maana yake katika Sarufi ya Kiswahili

View through CrossRef
Nomino sahili ni maneno ambayo kimofolojia yameundwa na mofu huru moja. Pia, kisematiki, maneno haya yana maana zake katika kamusi. Licha ya kuwa na sifa hizi, uambikaji wa viambishi ngeli {m-/mu-, ji-, ma-, ki-, ka-, tu, na u-} katika nomino hizi unaathiri sifa tajwa. Makala haya yanafafanua athari za kimofolojia na za kisemantiki za uambikaji wa viambishi ngeli katika nomino hizi na maana ya athari hizo katika ufafanuzi wa sarufi ya Kiswahili. Data zilizotumika zilipatikana kwa njia ya ushuhudiaji shiriki, hojaji na usaili. Data hizo zilifafanuliwa kwa kutumia Nadharia ya Matumizi iliyoasisiwa na Lodwig Wittgenstein (1953). Kutokana na data hizo, makala yanaonesha kwamba uambikaji wa viambishi ngeli kwenye nomino hizi husababisha athari za kimofolojia kama vile kuongeza idadi ya mofu kutoka moja kuwa mbili na kubadili aina ya nomino kimuundo. Vilevile, uambikaji huo huathiri maana ya nomino hizo kisarufi na kileksika kwa kuzingatia matumizi yake. Iwapo nomino hizi zitaendelea kupata mashiko na kisha kusanifiwa, athari tajwa zinadokeza mahitaji ya kuboresha uainishaji wa ngeli za nomino, uandikaji wa taarifa za vidahizo katika kamusi na ufafanuzi wa upanuzi na mabadiliko ya maana katika sarufi ya Kiswahili. Hivyo, imehitimishwa kwamba athari za kimofolojia na kisemantiki zinazotokana na uambikaji wa viambishi ngeli katika nomino sahili zinadhihirisha mabadiliko ya lugha na kwamba mabadiliko haya yanapaswa kuzingatiwa katika ufafanuzi wa sarufi ya Kiswahili. Kutokana na matokeo haya, imependekezwa kwamba zifanyike tafiti kuhusu uambikaji wa viambishi ngeli katika nomino sahili za makundi mengine ya nomino katika lugha ya Kiswahili.
University of Dar es Salaam
Title: Uambikaji wa Viambishi Ngeli katika Nomino Sahili Zinazorejelea Ndugu na Maana yake katika Sarufi ya Kiswahili
Description:
Nomino sahili ni maneno ambayo kimofolojia yameundwa na mofu huru moja.
Pia, kisematiki, maneno haya yana maana zake katika kamusi.
Licha ya kuwa na sifa hizi, uambikaji wa viambishi ngeli {m-/mu-, ji-, ma-, ki-, ka-, tu, na u-} katika nomino hizi unaathiri sifa tajwa.
Makala haya yanafafanua athari za kimofolojia na za kisemantiki za uambikaji wa viambishi ngeli katika nomino hizi na maana ya athari hizo katika ufafanuzi wa sarufi ya Kiswahili.
Data zilizotumika zilipatikana kwa njia ya ushuhudiaji shiriki, hojaji na usaili.
Data hizo zilifafanuliwa kwa kutumia Nadharia ya Matumizi iliyoasisiwa na Lodwig Wittgenstein (1953).
Kutokana na data hizo, makala yanaonesha kwamba uambikaji wa viambishi ngeli kwenye nomino hizi husababisha athari za kimofolojia kama vile kuongeza idadi ya mofu kutoka moja kuwa mbili na kubadili aina ya nomino kimuundo.
Vilevile, uambikaji huo huathiri maana ya nomino hizo kisarufi na kileksika kwa kuzingatia matumizi yake.
Iwapo nomino hizi zitaendelea kupata mashiko na kisha kusanifiwa, athari tajwa zinadokeza mahitaji ya kuboresha uainishaji wa ngeli za nomino, uandikaji wa taarifa za vidahizo katika kamusi na ufafanuzi wa upanuzi na mabadiliko ya maana katika sarufi ya Kiswahili.
Hivyo, imehitimishwa kwamba athari za kimofolojia na kisemantiki zinazotokana na uambikaji wa viambishi ngeli katika nomino sahili zinadhihirisha mabadiliko ya lugha na kwamba mabadiliko haya yanapaswa kuzingatiwa katika ufafanuzi wa sarufi ya Kiswahili.
Kutokana na matokeo haya, imependekezwa kwamba zifanyike tafiti kuhusu uambikaji wa viambishi ngeli katika nomino sahili za makundi mengine ya nomino katika lugha ya Kiswahili.

Related Results

Uraia, Lugha na Haki za Kidijitali: umuhimu wa lugha katika harakati za kuondoa ukoloni katika teknolojia
Uraia, Lugha na Haki za Kidijitali: umuhimu wa lugha katika harakati za kuondoa ukoloni katika teknolojia
Purpose Maneno mengi yanayohusu haki za binadamu na haki za kiteknolojia hayajatafsiriwa katika lugha ya Kiswahili. Kwa hivyo, wataalamu wa teknolojia na watetezi wa haki za kidiji...
Athari ya Ukosefu wa Ishara za Isimu katika Ufundishaji na Athari ya Mikato ya Kiingereza na Kiswahili katika Uchapishaji wa Vitabu
Athari ya Ukosefu wa Ishara za Isimu katika Ufundishaji na Athari ya Mikato ya Kiingereza na Kiswahili katika Uchapishaji wa Vitabu
Utafiti huu ulinuia kuchanganua usimilishaji wa ishara za isimu katika breili ya Kiswahili. Uchanganuzi huu ulitiwa hamasa na mambo matano muhimu. Kwanza, breili ndio njia ya pekee...
Vikwazo vya Usimilishaji wa Ishara za Isimu katika Breili
Vikwazo vya Usimilishaji wa Ishara za Isimu katika Breili
Utafiti huu ulinuia kuchanganua usimilishaji wa ishara za isimu katika breili ya Kiswahili. Uchanganuzi huu ulitiwa hamasa na mambo matano muhimu. Kwanza, breili ndio njia ya pekee...
Ujitokezaji wa Viarudhi vya Kifonolojia katika Kihaya: Uchunguzi Kifani wa Toni katika Lahaja ya Kihamba
Ujitokezaji wa Viarudhi vya Kifonolojia katika Kihaya: Uchunguzi Kifani wa Toni katika Lahaja ya Kihamba
Fonolojia ni taaluma iliyosheheni viarudhi au vipambasauti kama ambavyo wataalamu wengine huviita. Miongoni mwake ni toni, lafudhi, mkazo, nguvumsikiko, usilabi, kiimbo, unguvunguv...
Mapokezi ya Nomino za Kiswahili katika Ngeli za Nomino za Gᴉrᴉmi
Mapokezi ya Nomino za Kiswahili katika Ngeli za Nomino za Gᴉrᴉmi
Ikisiri Lengo la makala hii ni kuonesha jinsi nomino za Kiswahili zinavyokopwa ili kukidhi mawasiliano katika Gᴉrᴉmi. Nomino (majina) ni miongoni mwa maneno yanayokopwa kutokana na...
Ushairi WA Kiganda Unavyoweza Kuchangia Na Kuendeleza Ushairi WA Kiswahili Kimtindo Na Kimaudhui: Mfano WA Ufundishaji Nchini Uganda
Ushairi WA Kiganda Unavyoweza Kuchangia Na Kuendeleza Ushairi WA Kiswahili Kimtindo Na Kimaudhui: Mfano WA Ufundishaji Nchini Uganda
Wanafunzi wengi nchini Uganda wanachukulia utanzu wa ushairi wa Kiswahili kuwa mgumu na wanapata ugumu katika kujifunza ushairi wa Kiswahili. Ushairi wa Kiganda umekuwa unatendwa v...
Matumizi ya Kiswahili katika Mawasiliano na Uongozi wa Kidini katika Shule za Upili Nchini Kenya: Mfano wa Shule ya Wasichana ya Itigo
Matumizi ya Kiswahili katika Mawasiliano na Uongozi wa Kidini katika Shule za Upili Nchini Kenya: Mfano wa Shule ya Wasichana ya Itigo
Utafiti huu ulichunguza matumizi ya Kiswahili katika mawasiliano na uongozi wa kidini katika shule ya wasichana ya Itigo. Ulilenga kubaini jinsi lugha ya Kiswahili hutumika katika ...
Mabadiliko katika Mtaala wa Elimu ya Msingi na Namna Yanavyoathiri Tathmini katika Elimu ya Juu
Mabadiliko katika Mtaala wa Elimu ya Msingi na Namna Yanavyoathiri Tathmini katika Elimu ya Juu
Makala haya yamekusudia kuchunguza namna ambavyo mabadiliko katika mtaala wa elimu ya msingi yanavyoathiri tathmini katika elimu ya juu. Mabadiliko ya mtaala yanafanyika katika nga...

Back to Top