Search engine for discovering works of Art, research articles, and books related to Art and Culture
ShareThis
Javascript must be enabled to continue!

Athari za Mtaala wa Umilisi katika Ukuzaji wa Umahiri wa Kuzungumza Kiswahili kwa Wanafunzi wa Shule za Sekondari Nchini Uganda

View through CrossRef
Umahiri wa kuzungumza lugha ni miongoni mwa matokeo yanayotarajiwa kutoka kwa mtu yeyote anayejifunza lugha ya kigeni au lugha ya pili. Mathalani nchini Uganda imebainika kuwa kiwango cha umahiri wa kuzungumza Kiswahili kwa wanafunzi wa shule za sekondari kilikuwa cha chini sana licha ya kufundishwa lugha hiyo kwa kutumia Mtaala wa Maarifa. Utafiti wa awali uliofanywa na watafiti ulibainisha kuwa, kiwango cha umahiri cha wanafunzi kuzungumza lugha ya Kiswahili kimeongezeka tangu kuanza kutumiwa kwa Mtaala wa Umilisi katika ufundishaji mwaka 2020 tofauti na ilivyokuwa chini ya Mtaala wa Maarifa. Kutokana na matokeo hayo, utafiti uliozaa makala haya umetathmini athari za Mtaala wa Umilisi katika ukuzaji wa umahiri wa kuzungumza Kiswahili kwa wanafunzi wa shule za sekondari nchini Uganda. Sampuli ya watoataarifa kumi na wawili (12) walimu na ishirini na wanne (24) wanafunzi ilitumika kwenye utafiti huu. Nadharia ya Mawasiliano katika Ufundishaji wa Lugha imetumika katika uchanganuzi wa data za utafiti. Mbinu zilizotumika kukusanya data za utafiti huu ni ushuhudiaji na usaili. Matokeo ya utafiti huu yanaonesha kwamba, athari za Mtaala wa Umilisi katika ukuzaji wa umahiri wa kuzungumza Kiswahili imebainika kuwa mtaala una athari chanya. Athari hizo zipo katika mbinu za ufundishaji, mbinu za ujifunzaji, mawanda ya matumizi ya lugha ya Kiswahili kwa wanafunzi husika na mawanda ya ujifunzaji na tathmini.
Title: Athari za Mtaala wa Umilisi katika Ukuzaji wa Umahiri wa Kuzungumza Kiswahili kwa Wanafunzi wa Shule za Sekondari Nchini Uganda
Description:
Umahiri wa kuzungumza lugha ni miongoni mwa matokeo yanayotarajiwa kutoka kwa mtu yeyote anayejifunza lugha ya kigeni au lugha ya pili.
Mathalani nchini Uganda imebainika kuwa kiwango cha umahiri wa kuzungumza Kiswahili kwa wanafunzi wa shule za sekondari kilikuwa cha chini sana licha ya kufundishwa lugha hiyo kwa kutumia Mtaala wa Maarifa.
Utafiti wa awali uliofanywa na watafiti ulibainisha kuwa, kiwango cha umahiri cha wanafunzi kuzungumza lugha ya Kiswahili kimeongezeka tangu kuanza kutumiwa kwa Mtaala wa Umilisi katika ufundishaji mwaka 2020 tofauti na ilivyokuwa chini ya Mtaala wa Maarifa.
Kutokana na matokeo hayo, utafiti uliozaa makala haya umetathmini athari za Mtaala wa Umilisi katika ukuzaji wa umahiri wa kuzungumza Kiswahili kwa wanafunzi wa shule za sekondari nchini Uganda.
Sampuli ya watoataarifa kumi na wawili (12) walimu na ishirini na wanne (24) wanafunzi ilitumika kwenye utafiti huu.
Nadharia ya Mawasiliano katika Ufundishaji wa Lugha imetumika katika uchanganuzi wa data za utafiti.
Mbinu zilizotumika kukusanya data za utafiti huu ni ushuhudiaji na usaili.
Matokeo ya utafiti huu yanaonesha kwamba, athari za Mtaala wa Umilisi katika ukuzaji wa umahiri wa kuzungumza Kiswahili imebainika kuwa mtaala una athari chanya.
Athari hizo zipo katika mbinu za ufundishaji, mbinu za ujifunzaji, mawanda ya matumizi ya lugha ya Kiswahili kwa wanafunzi husika na mawanda ya ujifunzaji na tathmini.

Related Results

Visababishi vya Idadi Kubwa ya Wanafunzi wa Shule za Sekondari Nchini Uganda Kutochukua Somo la Kiswahili
Visababishi vya Idadi Kubwa ya Wanafunzi wa Shule za Sekondari Nchini Uganda Kutochukua Somo la Kiswahili
Katika makala haya, mtafiti anaeleza visababishi vya idadi kubwa ya wanafunzi katika shule za upili nchini Uganda kutochukua somo la Kiswahili. Wakati wa kupunguza idadi ya masomo ...
Mabadiliko katika Mtaala wa Elimu ya Msingi na Namna Yanavyoathiri Tathmini katika Elimu ya Juu
Mabadiliko katika Mtaala wa Elimu ya Msingi na Namna Yanavyoathiri Tathmini katika Elimu ya Juu
Makala haya yamekusudia kuchunguza namna ambavyo mabadiliko katika mtaala wa elimu ya msingi yanavyoathiri tathmini katika elimu ya juu. Mabadiliko ya mtaala yanafanyika katika nga...
Nafasi ya Kiswahili katika Ujenzi wa Utamaduni wa Uongozi katika Shule ya Msingi ya Mungakha, Kaunti ya Kakamega, Kenya
Nafasi ya Kiswahili katika Ujenzi wa Utamaduni wa Uongozi katika Shule ya Msingi ya Mungakha, Kaunti ya Kakamega, Kenya
Swahili Lengo la makala haya ni kupambanua nafasi ya Kiswahili katika ujenzi wa utamaduni wa uongozi katika Shule ya Msingi ya Mungakha, Kaunti ya Kakamega, nchini Kenya. Uongozi w...
Athari ya Ukosefu wa Ishara za Isimu katika Ufundishaji na Athari ya Mikato ya Kiingereza na Kiswahili katika Uchapishaji wa Vitabu
Athari ya Ukosefu wa Ishara za Isimu katika Ufundishaji na Athari ya Mikato ya Kiingereza na Kiswahili katika Uchapishaji wa Vitabu
Utafiti huu ulinuia kuchanganua usimilishaji wa ishara za isimu katika breili ya Kiswahili. Uchanganuzi huu ulitiwa hamasa na mambo matano muhimu. Kwanza, breili ndio njia ya pekee...
Matumizi ya Kiswahili katika Mawasiliano na Uongozi wa Kidini katika Shule za Upili Nchini Kenya: Mfano wa Shule ya Wasichana ya Itigo
Matumizi ya Kiswahili katika Mawasiliano na Uongozi wa Kidini katika Shule za Upili Nchini Kenya: Mfano wa Shule ya Wasichana ya Itigo
Utafiti huu ulichunguza matumizi ya Kiswahili katika mawasiliano na uongozi wa kidini katika shule ya wasichana ya Itigo. Ulilenga kubaini jinsi lugha ya Kiswahili hutumika katika ...
Umuhimu Wa Kufundisha Lugha Ya Kiswahili Katika Shule Za Sekondari Nchini Uganda
Umuhimu Wa Kufundisha Lugha Ya Kiswahili Katika Shule Za Sekondari Nchini Uganda
Katika makala haya, mtafiti anaeleza namna ambavyo Kiswahili kinaweza kuwa na manufaa kwa nchi ya Uganda. Ni kweli kwamba nchini Uganda, watu kadhaa wakiwemo baadhi ya wanasiasa ha...
Vikwazo vya Usimilishaji wa Ishara za Isimu katika Breili
Vikwazo vya Usimilishaji wa Ishara za Isimu katika Breili
Utafiti huu ulinuia kuchanganua usimilishaji wa ishara za isimu katika breili ya Kiswahili. Uchanganuzi huu ulitiwa hamasa na mambo matano muhimu. Kwanza, breili ndio njia ya pekee...
Maoni ya wanafunzi wa taasisi za kiufundi za kitaifa kuhusu nafasi ya Kiswahili katika elimu ya ufundi nchini Kenya
Maoni ya wanafunzi wa taasisi za kiufundi za kitaifa kuhusu nafasi ya Kiswahili katika elimu ya ufundi nchini Kenya
Utafiti huu ulinuia kutafuta maoni ya wanafunzi wa taasisi za kiufundi za kitaifa kuhusu nafasi ya lugha ya Kiswahili katika elimu ya kiufundi. Muundo wa Uchunguzi Kimaelezo ulitum...

Back to Top