Javascript must be enabled to continue!
Mabadiliko katika Mtaala wa Elimu ya Msingi na Namna Yanavyoathiri Tathmini katika Elimu ya Juu
View through CrossRef
Makala haya yamekusudia kuchunguza namna ambavyo mabadiliko katika mtaala wa elimu ya msingi yanavyoathiri tathmini katika elimu ya juu. Mabadiliko ya mtaala yanafanyika katika ngazi ya kitaifa nchini Kenya ambapo mfumo wa elimu wa 8-4-4 unaondolewa na nafasi yake kuchukuliwa na mtaala wa umilisi (CBC). Mabadiliko haya yamejikita katika elimu ya msingi, kuanzia kiwango cha chekechea, shule za upili hadi kwenye vyuo vinavyotoa elimu ya kiufundi kote nchini. Kwa sasa, mabadiliko katika mtaala wa kitaifa hayajaathiri vyuo vikuu kunakotolewa elimu ya juu. Hata hivyo, wanafunzi wanaojiunga na vyuo vikuu huandaliwa kupitia kwa mafunzo ya shule za upili. Hivyo basi mabadiliko yoyote yanayotokea katika elimu ya msingi lazima yataathiri programu za mafunzo yanayotolewa katika vyuo vikuu. Makala haya yataangazia kipengele cha tathmini katika vyuo vikuu kwa kuzingatia mabadiliko katika mfumo wa elimu uliopo na vigezo vinavyoelekeza tathmini katika mfumo wa elimu wa umilisi. Mabadiliko katika tathmini katika mfumo wa elimu wa umilisi yanaashiria kuwepo haja ya kufanya mabadiliko sawia ya tathmini katika mafunzo ya elimu ya juu katika vyuo vikuu. Hali hii inatokea kuwa hivi kwa kuwa wanafunzi wanapojiunga na vyuo vikuu watakuwa wamezoeshwa tathmini ya shule za upili ambayo hufanyika katika kila hatua ya ujifunzaji mafunzo yanapoendelea tofauti na illivyokuwa awali ambapo tathmini ilifanyika mara moja mwishoni baada ya kipindi maalumu cha mafunzo (mwishoni mwa miaka minane katika shule za msingi na miaka minne katika shule za upili). Swali hapa ni je, tathmini ya awali iliyozoeleka na ambayo ilifanyika baada ya kipindi maalumu bado itafaa? Bado itafikia malengo yaliyopo ya elimu? Kufikia sasa, hakuna mwelekeo wowote ambao umetolewa kuhusiana na hili. Hali hii inapelekea kuwepo haja ya kubuni sera itakayotoa mwelekeo kuhusu vigezo vinavyofaa kuzingatiwa katika kubadili tathmini katika vyuo vikuu ili iendane na mabadiliko yanayoendelea kutokea katika mfumo wa elimu uliopo. Mabadiliko katika tathmini vyuoni yanaweza kufanyika kwa kulinganisha na kulinganua tathmini iliyokuwepo awali na iliyopo hivi sasa katika elimu ya msingi na vyuo vikuu. Makala haya yamechanganua changamoto zinazotokana na hiyo mifumo miwili ya tathmini na kuangazia namna ambavyo aina zote mbili za tathmini humwathiri mwanafunzi ambaye ndiye mwathiriwa mkuu. Makala haya yamelenga kuwezesha vyuo vikuu kutambua mielekeo na mitazamo ambayo wanafunzi wanaotarajiwa kujiunga navyo huingia nayo vyuoni kutokana na namna wanavyotathminiwa wanapopokea elimu ya msingi. Makala haya yametokana na uchambuzi na mapitio ya maandishi yaliyopo tayari kuhusu mifumo hii miwili ya elimu pamoja na maoni ya wataalamu wa masuala ya mitaala. Maandishi haya yalipatikana maktabani na mitandaoni.
East African Nature and Science Organization
Title: Mabadiliko katika Mtaala wa Elimu ya Msingi na Namna Yanavyoathiri Tathmini katika Elimu ya Juu
Description:
Makala haya yamekusudia kuchunguza namna ambavyo mabadiliko katika mtaala wa elimu ya msingi yanavyoathiri tathmini katika elimu ya juu.
Mabadiliko ya mtaala yanafanyika katika ngazi ya kitaifa nchini Kenya ambapo mfumo wa elimu wa 8-4-4 unaondolewa na nafasi yake kuchukuliwa na mtaala wa umilisi (CBC).
Mabadiliko haya yamejikita katika elimu ya msingi, kuanzia kiwango cha chekechea, shule za upili hadi kwenye vyuo vinavyotoa elimu ya kiufundi kote nchini.
Kwa sasa, mabadiliko katika mtaala wa kitaifa hayajaathiri vyuo vikuu kunakotolewa elimu ya juu.
Hata hivyo, wanafunzi wanaojiunga na vyuo vikuu huandaliwa kupitia kwa mafunzo ya shule za upili.
Hivyo basi mabadiliko yoyote yanayotokea katika elimu ya msingi lazima yataathiri programu za mafunzo yanayotolewa katika vyuo vikuu.
Makala haya yataangazia kipengele cha tathmini katika vyuo vikuu kwa kuzingatia mabadiliko katika mfumo wa elimu uliopo na vigezo vinavyoelekeza tathmini katika mfumo wa elimu wa umilisi.
Mabadiliko katika tathmini katika mfumo wa elimu wa umilisi yanaashiria kuwepo haja ya kufanya mabadiliko sawia ya tathmini katika mafunzo ya elimu ya juu katika vyuo vikuu.
Hali hii inatokea kuwa hivi kwa kuwa wanafunzi wanapojiunga na vyuo vikuu watakuwa wamezoeshwa tathmini ya shule za upili ambayo hufanyika katika kila hatua ya ujifunzaji mafunzo yanapoendelea tofauti na illivyokuwa awali ambapo tathmini ilifanyika mara moja mwishoni baada ya kipindi maalumu cha mafunzo (mwishoni mwa miaka minane katika shule za msingi na miaka minne katika shule za upili).
Swali hapa ni je, tathmini ya awali iliyozoeleka na ambayo ilifanyika baada ya kipindi maalumu bado itafaa? Bado itafikia malengo yaliyopo ya elimu? Kufikia sasa, hakuna mwelekeo wowote ambao umetolewa kuhusiana na hili.
Hali hii inapelekea kuwepo haja ya kubuni sera itakayotoa mwelekeo kuhusu vigezo vinavyofaa kuzingatiwa katika kubadili tathmini katika vyuo vikuu ili iendane na mabadiliko yanayoendelea kutokea katika mfumo wa elimu uliopo.
Mabadiliko katika tathmini vyuoni yanaweza kufanyika kwa kulinganisha na kulinganua tathmini iliyokuwepo awali na iliyopo hivi sasa katika elimu ya msingi na vyuo vikuu.
Makala haya yamechanganua changamoto zinazotokana na hiyo mifumo miwili ya tathmini na kuangazia namna ambavyo aina zote mbili za tathmini humwathiri mwanafunzi ambaye ndiye mwathiriwa mkuu.
Makala haya yamelenga kuwezesha vyuo vikuu kutambua mielekeo na mitazamo ambayo wanafunzi wanaotarajiwa kujiunga navyo huingia nayo vyuoni kutokana na namna wanavyotathminiwa wanapopokea elimu ya msingi.
Makala haya yametokana na uchambuzi na mapitio ya maandishi yaliyopo tayari kuhusu mifumo hii miwili ya elimu pamoja na maoni ya wataalamu wa masuala ya mitaala.
Maandishi haya yalipatikana maktabani na mitandaoni.
Related Results
Mustakabali wa Kiswahili kama Lugha ya Kufundishia Nchini Tanzania: Uhakiki wa Maudhui ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya 2014
Mustakabali wa Kiswahili kama Lugha ya Kufundishia Nchini Tanzania: Uhakiki wa Maudhui ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya 2014
Msingi wa makala haya ni “Sera ya Elimu na Mafunzo” (SEM, 2014). Makala yanahakiki nafasi ya lugha ya Kiswahili kwenye Sera ya Elimu na Mafunzo nchini Tanzania na mustakabali wake ...
Uambikaji wa Viambishi Ngeli katika Nomino Sahili Zinazorejelea Ndugu na Maana yake katika Sarufi ya Kiswahili
Uambikaji wa Viambishi Ngeli katika Nomino Sahili Zinazorejelea Ndugu na Maana yake katika Sarufi ya Kiswahili
Nomino sahili ni maneno ambayo kimofolojia yameundwa na mofu huru moja. Pia, kisematiki, maneno haya yana maana zake katika kamusi. Licha ya kuwa na sifa hizi, uambikaji wa viambis...
Jinsi Masuala ya Kijinsia Yalivyo Shughulikiwa Katika Tamthilia ya ‘Bembea ya Maisha’ kwa Kuzingatia Jinsia ya Mwandishi
Jinsi Masuala ya Kijinsia Yalivyo Shughulikiwa Katika Tamthilia ya ‘Bembea ya Maisha’ kwa Kuzingatia Jinsia ya Mwandishi
Maumbile ya binadamu yamechukua mikondo miwili; mwanamume na mwanamke. Jamii tofauti hutoa majukumu kwa kuzingatia migao hii miwili. Hivi ni kusema kuwa, shughuli za mtu katika jam...
Athari ya Mitindo Mbalimbali ya Breili katika Unukuzi wa Maandishi ya Breili ya Kiswahili
Athari ya Mitindo Mbalimbali ya Breili katika Unukuzi wa Maandishi ya Breili ya Kiswahili
Utafiti huu ulinuia kuchanganua usahihi wa unukuzi wa maandishi ya breili hadi maandishi ya kawaida na kinyume chake, ili kuleta maana iliyokusudiwa. Katika kutimiza lengo hilo, ut...
Matumizi ya Lugha Kwenye Malezi ya Watoto: Mfano wa Matumizi ya Semi Katika Jamii ya Wamasaaba Nchini Uganda
Matumizi ya Lugha Kwenye Malezi ya Watoto: Mfano wa Matumizi ya Semi Katika Jamii ya Wamasaaba Nchini Uganda
Katika makala haya, mtafiti anaeleza jinsi lugha inavyotumiwa na wazazi katika shughuli yao ya kulea watoto. Alifanya hivyo kwa kurejelea malezi ya watoto katika jamii ya Wamasaaba...
Nafasi ya Riwaya za Kingano za Kiswahili katika Harakati za Kupigania Hadhi-Msingi ya Mwanamke. Mfano Riwaya ya Marimba ya Majaliwa (2008) ya Edwin Semzaba
Nafasi ya Riwaya za Kingano za Kiswahili katika Harakati za Kupigania Hadhi-Msingi ya Mwanamke. Mfano Riwaya ya Marimba ya Majaliwa (2008) ya Edwin Semzaba
Makala haya yanalenga kuonesha namna riwaya za kingano za Kiswahili zinavyoweza kutumika kumpigania na kumkomboa mtu mnyonge hususani mwanamke na mtoto. Baadhi ya watu wanadhani ng...
Mchango wa Mikakati ya Upole Katika Mazungumzo ya ibada ya Mazishi katika Lugha ya Kikabrasi
Mchango wa Mikakati ya Upole Katika Mazungumzo ya ibada ya Mazishi katika Lugha ya Kikabrasi
Swahili
Suala la upole limetafitiwa na wasomi wengi kwenye mawasiliano, ikiwemo mazungumzo ya abiria na wahudumu wa magari ya uchukuzi kwa lugha ya Kikamba. Hata hivyo, utafiti huu...
Propaganda Kama Mkakati wa Kuhimili Hejemonia: Mfano wa Dharau ya Ini, Msimu wa Vipepeo, Msururu wa Usaliti na Majilio ya Mkombozi
Propaganda Kama Mkakati wa Kuhimili Hejemonia: Mfano wa Dharau ya Ini, Msimu wa Vipepeo, Msururu wa Usaliti na Majilio ya Mkombozi
Makala hii imechunguza suala la propaganda kama mkakati wa kuhimili hejemonia katika riwaya teule za Kiswahili. Mtafiti amejadili namna propaganda inatumiwa kudumisha na kuimarisha...

