Search engine for discovering works of Art, research articles, and books related to Art and Culture
ShareThis
Javascript must be enabled to continue!

Athari ya Mitindo Mbalimbali ya Breili katika Unukuzi wa Maandishi ya Breili ya Kiswahili

View through CrossRef
Utafiti huu ulinuia kuchanganua usahihi wa unukuzi wa maandishi ya breili hadi maandishi ya kawaida na kinyume chake, ili kuleta maana iliyokusudiwa. Katika kutimiza lengo hilo, utafiti huu umechunguza changamoto au ugumu wanaokumbana nao wanukuzi wa maandishi haya na athari yake kwa wanafunzi wasioona katika elimu. Utafiti wa nyanjani ndio uliofaa kazi hii, nazo mbinu za kukusanya data zilizozofaa ni hojaji na mahojiano. Wanafunzi walipewa kazi ya kuandika insha zilizopewa wanukuzi walizozinukuu ili kuchanganuliwa. Uchunguzi huu ulikusudiwa kufanywa katika vyuo vya elimu kama vile Chuo Kikuu cha Kenyatta, Chuo Kikuu cha Maseno, Taasisi ya Elimu ya Machakos, Taasisi ya Wasioona ya Kenya na Taasisi ya Elimu ya Kagumo kwa sababu vyuo  hivi ndivyo vilivyo na wahadhiri wengi wasiojua kusoma breili na mara nyingi husaidiwa na wanukuzi kunukuu kazi za breili katika maandishi ya kawaida ili wakapate kusoma na kuelewa. Kutokana na utafiti huu ni wazi kuwa tafsiri ya breili ya Kiswahili hadi maandishi ya kawaida imepungukiwa katika kuwasilisha maana iliyokusudiwa kwa sababu ya ukosefu wa breili sanifu ya Kiswahili, kuwepo kwa changamoto zilizofafanuliwa katika tasnifu hii na ukosefu wa umilisi katika breili ya Kiswahili miongoni mwa wanafunzi na wanukuzi huathiri pakubwa tafsiri ya maandishi haya. Utafiti huu utawanufaisha wanaotumia breili, walimu wao na wanukuzi wa maandishi haya ya breili
East African Nature and Science Organization
Title: Athari ya Mitindo Mbalimbali ya Breili katika Unukuzi wa Maandishi ya Breili ya Kiswahili
Description:
Utafiti huu ulinuia kuchanganua usahihi wa unukuzi wa maandishi ya breili hadi maandishi ya kawaida na kinyume chake, ili kuleta maana iliyokusudiwa.
Katika kutimiza lengo hilo, utafiti huu umechunguza changamoto au ugumu wanaokumbana nao wanukuzi wa maandishi haya na athari yake kwa wanafunzi wasioona katika elimu.
Utafiti wa nyanjani ndio uliofaa kazi hii, nazo mbinu za kukusanya data zilizozofaa ni hojaji na mahojiano.
Wanafunzi walipewa kazi ya kuandika insha zilizopewa wanukuzi walizozinukuu ili kuchanganuliwa.
Uchunguzi huu ulikusudiwa kufanywa katika vyuo vya elimu kama vile Chuo Kikuu cha Kenyatta, Chuo Kikuu cha Maseno, Taasisi ya Elimu ya Machakos, Taasisi ya Wasioona ya Kenya na Taasisi ya Elimu ya Kagumo kwa sababu vyuo  hivi ndivyo vilivyo na wahadhiri wengi wasiojua kusoma breili na mara nyingi husaidiwa na wanukuzi kunukuu kazi za breili katika maandishi ya kawaida ili wakapate kusoma na kuelewa.
Kutokana na utafiti huu ni wazi kuwa tafsiri ya breili ya Kiswahili hadi maandishi ya kawaida imepungukiwa katika kuwasilisha maana iliyokusudiwa kwa sababu ya ukosefu wa breili sanifu ya Kiswahili, kuwepo kwa changamoto zilizofafanuliwa katika tasnifu hii na ukosefu wa umilisi katika breili ya Kiswahili miongoni mwa wanafunzi na wanukuzi huathiri pakubwa tafsiri ya maandishi haya.
Utafiti huu utawanufaisha wanaotumia breili, walimu wao na wanukuzi wa maandishi haya ya breili.

Related Results

Vikwazo vya Usimilishaji wa Ishara za Isimu katika Breili
Vikwazo vya Usimilishaji wa Ishara za Isimu katika Breili
Utafiti huu ulinuia kuchanganua usimilishaji wa ishara za isimu katika breili ya Kiswahili. Uchanganuzi huu ulitiwa hamasa na mambo matano muhimu. Kwanza, breili ndio njia ya pekee...
Athari ya Ukosefu wa Ishara za Isimu katika Ufundishaji na Athari ya Mikato ya Kiingereza na Kiswahili katika Uchapishaji wa Vitabu
Athari ya Ukosefu wa Ishara za Isimu katika Ufundishaji na Athari ya Mikato ya Kiingereza na Kiswahili katika Uchapishaji wa Vitabu
Utafiti huu ulinuia kuchanganua usimilishaji wa ishara za isimu katika breili ya Kiswahili. Uchanganuzi huu ulitiwa hamasa na mambo matano muhimu. Kwanza, breili ndio njia ya pekee...
Uraia, Lugha na Haki za Kidijitali: umuhimu wa lugha katika harakati za kuondoa ukoloni katika teknolojia
Uraia, Lugha na Haki za Kidijitali: umuhimu wa lugha katika harakati za kuondoa ukoloni katika teknolojia
Purpose Maneno mengi yanayohusu haki za binadamu na haki za kiteknolojia hayajatafsiriwa katika lugha ya Kiswahili. Kwa hivyo, wataalamu wa teknolojia na watetezi wa haki za kidiji...
Mabadiliko katika Mtaala wa Elimu ya Msingi na Namna Yanavyoathiri Tathmini katika Elimu ya Juu
Mabadiliko katika Mtaala wa Elimu ya Msingi na Namna Yanavyoathiri Tathmini katika Elimu ya Juu
Makala haya yamekusudia kuchunguza namna ambavyo mabadiliko katika mtaala wa elimu ya msingi yanavyoathiri tathmini katika elimu ya juu. Mabadiliko ya mtaala yanafanyika katika nga...
Ubainishaji wa Vipengele vya Ujumi wa Kiafrika na Athari yake katika Ushairi wa Kiswahili: Uchunguzi wa Ushairi wa Bongo Fleva
Ubainishaji wa Vipengele vya Ujumi wa Kiafrika na Athari yake katika Ushairi wa Kiswahili: Uchunguzi wa Ushairi wa Bongo Fleva
Makala haya yalichunguza ujitokezaji wa ujumi wa Kiafrika katika ushairi wa Kiswahili wa Bongo Fleva pamoja na athari yake katika ushairi huo. Tafiti kuhusu vipengele vya ujumi wa ...
Ushairi WA Kiganda Unavyoweza Kuchangia Na Kuendeleza Ushairi WA Kiswahili Kimtindo Na Kimaudhui: Mfano WA Ufundishaji Nchini Uganda
Ushairi WA Kiganda Unavyoweza Kuchangia Na Kuendeleza Ushairi WA Kiswahili Kimtindo Na Kimaudhui: Mfano WA Ufundishaji Nchini Uganda
Wanafunzi wengi nchini Uganda wanachukulia utanzu wa ushairi wa Kiswahili kuwa mgumu na wanapata ugumu katika kujifunza ushairi wa Kiswahili. Ushairi wa Kiganda umekuwa unatendwa v...
Ujitokezaji wa Viarudhi vya Kifonolojia katika Kihaya: Uchunguzi Kifani wa Toni katika Lahaja ya Kihamba
Ujitokezaji wa Viarudhi vya Kifonolojia katika Kihaya: Uchunguzi Kifani wa Toni katika Lahaja ya Kihamba
Fonolojia ni taaluma iliyosheheni viarudhi au vipambasauti kama ambavyo wataalamu wengine huviita. Miongoni mwake ni toni, lafudhi, mkazo, nguvumsikiko, usilabi, kiimbo, unguvunguv...
Matumizi ya Kiswahili katika Mawasiliano na Uongozi wa Kidini katika Shule za Upili Nchini Kenya: Mfano wa Shule ya Wasichana ya Itigo
Matumizi ya Kiswahili katika Mawasiliano na Uongozi wa Kidini katika Shule za Upili Nchini Kenya: Mfano wa Shule ya Wasichana ya Itigo
Utafiti huu ulichunguza matumizi ya Kiswahili katika mawasiliano na uongozi wa kidini katika shule ya wasichana ya Itigo. Ulilenga kubaini jinsi lugha ya Kiswahili hutumika katika ...

Back to Top