Javascript must be enabled to continue!
Ufanano wa Mtoto wa Laana Kumuua Babaye katika Nyakiiru Kibi na Mfalme Edipode: Dhihiriko la Umageuko au Msambao?
View through CrossRef
Ikisiri
Kisa kinachoelezwa katika simulizi ya Edipode katika tamthilia ya Mfalme Edipode (Sofokile, 1971) kinafanana kwa karibu sana na kisa kinachosimuliwa katika Utenzi wa Nyakiiru Kibi (Mulokozi, 1998). Sababu kubwa zilizochangia kufanana kwa simulizi hizi mbili zinaweza kuelezwa kwa kuzingatia misingi ya kinadharia, hususan Nadharia ya Mageuko na Nadharia ya Msambao. Wakati Nadharia ya Mageuko ikidai kuwa simulizi yoyote ile ni matokeo ya mabadiliko ya ndani ya jamii yanayochagizwa na mazingira, Nadharia ya Msambao inasisitiza kuwa simulizi huenea kutoka sehemu moja hadi nyingine; kamwe haiwezekani simulizi mbili zinazofanana kuibuka katika jamii mbili ambazo hazijawahi kukutana. Makala hii imechunguza sababu za kufanana kwa visa katika simulizi teule kwa kutumia misingi ya nadharia hizo mbili. Kwa kuzingatia hoja mbalimbali, imehitimishwa kuwa simulizi ya Nyakiiru Kibi, pamoja na kutungwa takribani karne 24 baada ya ile ya Edipode, si kiatani cha Edipode. Simulizi hii imechimbuka katika eneo la Maziwa Makuu na inaonekana ni tukio linalofungamana na historia ya jamii husika huku ikijumuisha visakale hapa na pale.
Title: Ufanano wa Mtoto wa Laana Kumuua Babaye katika Nyakiiru Kibi na Mfalme Edipode: Dhihiriko la Umageuko au Msambao?
Description:
Ikisiri
Kisa kinachoelezwa katika simulizi ya Edipode katika tamthilia ya Mfalme Edipode (Sofokile, 1971) kinafanana kwa karibu sana na kisa kinachosimuliwa katika Utenzi wa Nyakiiru Kibi (Mulokozi, 1998).
Sababu kubwa zilizochangia kufanana kwa simulizi hizi mbili zinaweza kuelezwa kwa kuzingatia misingi ya kinadharia, hususan Nadharia ya Mageuko na Nadharia ya Msambao.
Wakati Nadharia ya Mageuko ikidai kuwa simulizi yoyote ile ni matokeo ya mabadiliko ya ndani ya jamii yanayochagizwa na mazingira, Nadharia ya Msambao inasisitiza kuwa simulizi huenea kutoka sehemu moja hadi nyingine; kamwe haiwezekani simulizi mbili zinazofanana kuibuka katika jamii mbili ambazo hazijawahi kukutana.
Makala hii imechunguza sababu za kufanana kwa visa katika simulizi teule kwa kutumia misingi ya nadharia hizo mbili.
Kwa kuzingatia hoja mbalimbali, imehitimishwa kuwa simulizi ya Nyakiiru Kibi, pamoja na kutungwa takribani karne 24 baada ya ile ya Edipode, si kiatani cha Edipode.
Simulizi hii imechimbuka katika eneo la Maziwa Makuu na inaonekana ni tukio linalofungamana na historia ya jamii husika huku ikijumuisha visakale hapa na pale.
Related Results
Mabadiliko katika Mtaala wa Elimu ya Msingi na Namna Yanavyoathiri Tathmini katika Elimu ya Juu
Mabadiliko katika Mtaala wa Elimu ya Msingi na Namna Yanavyoathiri Tathmini katika Elimu ya Juu
Makala haya yamekusudia kuchunguza namna ambavyo mabadiliko katika mtaala wa elimu ya msingi yanavyoathiri tathmini katika elimu ya juu. Mabadiliko ya mtaala yanafanyika katika nga...
Jinsi Masuala ya Kijinsia Yalivyo Shughulikiwa Katika Tamthilia ya ‘Bembea ya Maisha’ kwa Kuzingatia Jinsia ya Mwandishi
Jinsi Masuala ya Kijinsia Yalivyo Shughulikiwa Katika Tamthilia ya ‘Bembea ya Maisha’ kwa Kuzingatia Jinsia ya Mwandishi
Maumbile ya binadamu yamechukua mikondo miwili; mwanamume na mwanamke. Jamii tofauti hutoa majukumu kwa kuzingatia migao hii miwili. Hivi ni kusema kuwa, shughuli za mtu katika jam...
Nafasi ya Riwaya za Kingano za Kiswahili katika Harakati za Kupigania Hadhi-Msingi ya Mwanamke. Mfano Riwaya ya Marimba ya Majaliwa (2008) ya Edwin Semzaba
Nafasi ya Riwaya za Kingano za Kiswahili katika Harakati za Kupigania Hadhi-Msingi ya Mwanamke. Mfano Riwaya ya Marimba ya Majaliwa (2008) ya Edwin Semzaba
Makala haya yanalenga kuonesha namna riwaya za kingano za Kiswahili zinavyoweza kutumika kumpigania na kumkomboa mtu mnyonge hususani mwanamke na mtoto. Baadhi ya watu wanadhani ng...
Uambikaji wa Viambishi Ngeli katika Nomino Sahili Zinazorejelea Ndugu na Maana yake katika Sarufi ya Kiswahili
Uambikaji wa Viambishi Ngeli katika Nomino Sahili Zinazorejelea Ndugu na Maana yake katika Sarufi ya Kiswahili
Nomino sahili ni maneno ambayo kimofolojia yameundwa na mofu huru moja. Pia, kisematiki, maneno haya yana maana zake katika kamusi. Licha ya kuwa na sifa hizi, uambikaji wa viambis...
Matumizi ya Lugha Kwenye Malezi ya Watoto: Mfano wa Matumizi ya Semi Katika Jamii ya Wamasaaba Nchini Uganda
Matumizi ya Lugha Kwenye Malezi ya Watoto: Mfano wa Matumizi ya Semi Katika Jamii ya Wamasaaba Nchini Uganda
Katika makala haya, mtafiti anaeleza jinsi lugha inavyotumiwa na wazazi katika shughuli yao ya kulea watoto. Alifanya hivyo kwa kurejelea malezi ya watoto katika jamii ya Wamasaaba...
Mchango wa Mikakati ya Upole Katika Mazungumzo ya ibada ya Mazishi katika Lugha ya Kikabrasi
Mchango wa Mikakati ya Upole Katika Mazungumzo ya ibada ya Mazishi katika Lugha ya Kikabrasi
Swahili
Suala la upole limetafitiwa na wasomi wengi kwenye mawasiliano, ikiwemo mazungumzo ya abiria na wahudumu wa magari ya uchukuzi kwa lugha ya Kikamba. Hata hivyo, utafiti huu...
Mikakati ya Upole Katika Mawasiliano ya Wahudumu wa Magari ya Uchukuzi na Abiria katika lugha ya Kikamba.
Mikakati ya Upole Katika Mawasiliano ya Wahudumu wa Magari ya Uchukuzi na Abiria katika lugha ya Kikamba.
Upole ni hali ya msemaji kudhihirisha kuwa anajali hisia na mahitaji ya msikilizaji katika mazungumzo. Mikakati ya upole hutumiwa na washiriki wa mazungumzo kulainisha na kufanikis...
Matumizi ya Lugha katika Tamthiliya ya ( Sadaka ya John Okello )
Matumizi ya Lugha katika Tamthiliya ya ( Sadaka ya John Okello )
Kipengele hiki hakipatikani katika lugha zote (bonyeza chache tu). Grafu iliyotangulia Ni ngapi huduma hii haipatikani katika lugha zote. Chini ni orodha ya kurasa zetu maarufu za ...


