Javascript must be enabled to continue!
Tafsiri ya Lugha ya Ishara katika Wema Hawajazaliwa: Mtazamo wa Ulinganifu wa Kimawasiliano
View through CrossRef
Tafsiri ni taaluma kongwe ambayo imekuwa ikifanyika katika nyuga mbalimbali kama vile sheria, utabibu na lugha. Tafiti nyingi zimekitwa katika matatizo ya tafsiri kwa ujumla. Wataalamu wa tafsiri, hususani za kifasihi kama vile Mkinga (2005), Malangwa (2010) na Mekacha (2013), wametafiti kuhusu mbinu na matatizo ya kutafsiri matini za kifasihi. Data za makala hii zimetokana na mbinu ya uchambuzi wa matini na usaili. Wafasiri tofauti wametafsiri kazi za kifasihi kwa kuzingatia usanaa uliomo kwenye kazi husika. Makala hii inamulika tafsiri ya lugha ya ishara katika Wema Hawajazaliwa kwa kuzingatia mtazamo wa ulinganifu wa kimawasiliano. Wema Hawajazaliwa ni riwaya iliyotafsiriwa na Abdilatif Abdallah kutoka katika riwaya ya The Beautyful Ones are not Yet Born ya Ayi Kwei Armah. Makala hii iliongozwa na Nadharia ya Ulinganifu wa Kimawasiliano iliyoasisiwa na Nida (1964). Pamoja na wataalamu wengi kutafiti kuhusu matatizo ya tafsiri, bado tafsiri ya kifasihi haijafanyiwa tafiti za kutosha hususani katika lugha ya Kiswahili. Makala hii imebaini kuwa, mfasiri huzingatia lugha ya ishara katika tafsiri ya matukio mbalimbali ya kiishara.
Title: Tafsiri ya Lugha ya Ishara katika Wema Hawajazaliwa: Mtazamo wa Ulinganifu wa Kimawasiliano
Description:
Tafsiri ni taaluma kongwe ambayo imekuwa ikifanyika katika nyuga mbalimbali kama vile sheria, utabibu na lugha.
Tafiti nyingi zimekitwa katika matatizo ya tafsiri kwa ujumla.
Wataalamu wa tafsiri, hususani za kifasihi kama vile Mkinga (2005), Malangwa (2010) na Mekacha (2013), wametafiti kuhusu mbinu na matatizo ya kutafsiri matini za kifasihi.
Data za makala hii zimetokana na mbinu ya uchambuzi wa matini na usaili.
Wafasiri tofauti wametafsiri kazi za kifasihi kwa kuzingatia usanaa uliomo kwenye kazi husika.
Makala hii inamulika tafsiri ya lugha ya ishara katika Wema Hawajazaliwa kwa kuzingatia mtazamo wa ulinganifu wa kimawasiliano.
Wema Hawajazaliwa ni riwaya iliyotafsiriwa na Abdilatif Abdallah kutoka katika riwaya ya The Beautyful Ones are not Yet Born ya Ayi Kwei Armah.
Makala hii iliongozwa na Nadharia ya Ulinganifu wa Kimawasiliano iliyoasisiwa na Nida (1964).
Pamoja na wataalamu wengi kutafiti kuhusu matatizo ya tafsiri, bado tafsiri ya kifasihi haijafanyiwa tafiti za kutosha hususani katika lugha ya Kiswahili.
Makala hii imebaini kuwa, mfasiri huzingatia lugha ya ishara katika tafsiri ya matukio mbalimbali ya kiishara.
Related Results
Uraia, Lugha na Haki za Kidijitali: umuhimu wa lugha katika harakati za kuondoa ukoloni katika teknolojia
Uraia, Lugha na Haki za Kidijitali: umuhimu wa lugha katika harakati za kuondoa ukoloni katika teknolojia
Purpose
Maneno mengi yanayohusu haki za binadamu na haki za kiteknolojia hayajatafsiriwa katika lugha ya Kiswahili. Kwa hivyo, wataalamu wa teknolojia na watetezi wa haki za kidiji...
Mtunzi kama Mtafsiri Anayeingilia Kati ya Tafsiri: Kifo Kisimani (1999) na Natala (2005)
Mtunzi kama Mtafsiri Anayeingilia Kati ya Tafsiri: Kifo Kisimani (1999) na Natala (2005)
Utafiti huu unalenga kuchunguza kwa kina nafasi na athari za mwandishi anaposhiriki moja kwa moja katika mchakato wa kutafsiri kazi yake ya kifasihi, kwa kuzingatia tamthilia mbili...
Uamilifu wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Kimatumizi kwenye Kaunti ya Bungoma
Uamilifu wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Kimatumizi kwenye Kaunti ya Bungoma
Lugha ni chombo maalum katika ustawishaji na uimarishaji wa rasilimali za mwanadamu. Pia, ni wenzo unaohimili sera ambazo hulenga katika kutimiza matarajio ya kitaifa katika nchi y...
Vikwazo vya Usimilishaji wa Ishara za Isimu katika Breili
Vikwazo vya Usimilishaji wa Ishara za Isimu katika Breili
Utafiti huu ulinuia kuchanganua usimilishaji wa ishara za isimu katika breili ya Kiswahili. Uchanganuzi huu ulitiwa hamasa na mambo matano muhimu. Kwanza, breili ndio njia ya pekee...
Athari ya Ukosefu wa Ishara za Isimu katika Ufundishaji na Athari ya Mikato ya Kiingereza na Kiswahili katika Uchapishaji wa Vitabu
Athari ya Ukosefu wa Ishara za Isimu katika Ufundishaji na Athari ya Mikato ya Kiingereza na Kiswahili katika Uchapishaji wa Vitabu
Utafiti huu ulinuia kuchanganua usimilishaji wa ishara za isimu katika breili ya Kiswahili. Uchanganuzi huu ulitiwa hamasa na mambo matano muhimu. Kwanza, breili ndio njia ya pekee...
Vipengele Vya Fasihi Vinavyojenga Taswira Ya Mwanamke Katikavitabu Teule Vya Biblia Takatifu
Vipengele Vya Fasihi Vinavyojenga Taswira Ya Mwanamke Katikavitabu Teule Vya Biblia Takatifu
Lugha ni chombo cha kipekee kinachofinyangwa kuwasilisha taswira ya masuala changamano katika jamii. Matokeo haya ya lugha ni fasihi, ambayo ni kioo cha jamii. Biblia Takatifu ni k...
Matumizi ya Kiswahili katika Mawasiliano na Uongozi wa Kidini katika Shule za Upili Nchini Kenya: Mfano wa Shule ya Wasichana ya Itigo
Matumizi ya Kiswahili katika Mawasiliano na Uongozi wa Kidini katika Shule za Upili Nchini Kenya: Mfano wa Shule ya Wasichana ya Itigo
Utafiti huu ulichunguza matumizi ya Kiswahili katika mawasiliano na uongozi wa kidini katika shule ya wasichana ya Itigo. Ulilenga kubaini jinsi lugha ya Kiswahili hutumika katika ...
Nafasi ya Ikolojia ya Lugha katika Mtagusano wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Dini katika Kaunti ya Bungoma
Nafasi ya Ikolojia ya Lugha katika Mtagusano wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Dini katika Kaunti ya Bungoma
Nyanja mbalimbali katika jamii hutegemea matumizi ya lugha. Hali hii huzua changamoto ya namna ya kutumia raslimali za lugha zinazopatikana katika jamiilugha fulani. Juhudi ya kufa...

