Search engine for discovering works of Art, research articles, and books related to Art and Culture
ShareThis
Javascript must be enabled to continue!

Uundaji wa Maneno ya Kiswahili katika Mawasiliano Mahalia: Utafiti wa Lugha za Kundi F30

View through CrossRef
Uundaji wa maneno hulenga kukidhi mawasiliano kufuatia kujitokeza kwa mapengo ya mawasiliano, aghalabu, yanayosababishwa na kuzuka kwa vitu vipya au kukutana kwa makundi lugha mawili au zaidi yanayohitaji kuwasiliana na kuelewana. Makala hii inahusu uundaji wa maneno ya Kiswahili pale jamiilugha za Kundi F30, ambazo ni Wanyiramba (F31), Wanyaturu (F32) na Warangi (F33), zinapowasiliana kwa Kiswahili kwa lengo la kukidhi mawasiliano. Makala hii imeshughulikia malengo mawili ambayo ni kubainisha maneno ya Kiswahili yanayoundwa katika jamiilugha za Kundi F30 na kufafanua mbinu zinazotumika kuunda maneno hayo. Nadharia ya Usilimishaji ilitumika katika uchambuzi na mjadala wa matokeo. Mbinu zilizotumika kukusanya data ni usaili na uchambuzi matini. Matokeo ya utafiti yanaonesha kuwa, pale wazungumzaji wa lugha mahususi za Kundi F30 wanapowasiliana wao kwa wao, hutumia maneno ya asili kutaja majina hayo, lakini wanapowasiliana kwa Kiswahili, hutumia maneno ya Kiswahili yanayofahamika ndani ya kundi hilo pana. Imeonekana zaidi kuwa maneno hayo huundwa kwa kutumia kanuni nne ambazo ni unasibu, utohoaji, uhamishaji na ukarabati-maana. Kufuatia matokeo hayo, makala hii inapendekeza kwamba maneno ya Kiswahili mahalia yakusanywe na kutambuliwa kwa kuingizwa katika kamusi mahususi za Kiswahili ili jamii pana ya Waswahili iweze kunufaika nayo.
University of Dar es Salaam
Title: Uundaji wa Maneno ya Kiswahili katika Mawasiliano Mahalia: Utafiti wa Lugha za Kundi F30
Description:
Uundaji wa maneno hulenga kukidhi mawasiliano kufuatia kujitokeza kwa mapengo ya mawasiliano, aghalabu, yanayosababishwa na kuzuka kwa vitu vipya au kukutana kwa makundi lugha mawili au zaidi yanayohitaji kuwasiliana na kuelewana.
Makala hii inahusu uundaji wa maneno ya Kiswahili pale jamiilugha za Kundi F30, ambazo ni Wanyiramba (F31), Wanyaturu (F32) na Warangi (F33), zinapowasiliana kwa Kiswahili kwa lengo la kukidhi mawasiliano.
Makala hii imeshughulikia malengo mawili ambayo ni kubainisha maneno ya Kiswahili yanayoundwa katika jamiilugha za Kundi F30 na kufafanua mbinu zinazotumika kuunda maneno hayo.
Nadharia ya Usilimishaji ilitumika katika uchambuzi na mjadala wa matokeo.
Mbinu zilizotumika kukusanya data ni usaili na uchambuzi matini.
Matokeo ya utafiti yanaonesha kuwa, pale wazungumzaji wa lugha mahususi za Kundi F30 wanapowasiliana wao kwa wao, hutumia maneno ya asili kutaja majina hayo, lakini wanapowasiliana kwa Kiswahili, hutumia maneno ya Kiswahili yanayofahamika ndani ya kundi hilo pana.
Imeonekana zaidi kuwa maneno hayo huundwa kwa kutumia kanuni nne ambazo ni unasibu, utohoaji, uhamishaji na ukarabati-maana.
Kufuatia matokeo hayo, makala hii inapendekeza kwamba maneno ya Kiswahili mahalia yakusanywe na kutambuliwa kwa kuingizwa katika kamusi mahususi za Kiswahili ili jamii pana ya Waswahili iweze kunufaika nayo.

Related Results

Uraia, Lugha na Haki za Kidijitali: umuhimu wa lugha katika harakati za kuondoa ukoloni katika teknolojia
Uraia, Lugha na Haki za Kidijitali: umuhimu wa lugha katika harakati za kuondoa ukoloni katika teknolojia
Purpose Maneno mengi yanayohusu haki za binadamu na haki za kiteknolojia hayajatafsiriwa katika lugha ya Kiswahili. Kwa hivyo, wataalamu wa teknolojia na watetezi wa haki za kidiji...
Maneno katika S. E. D. ambayo Hutumika katika Kiswahili Sanifu
Maneno katika S. E. D. ambayo Hutumika katika Kiswahili Sanifu
Utafiti huu ulidhamiria kutathmini athari za kamusi ya Sheng’ – English Dictionary kwa Kiswahili sanifu. Kamusi ya Sheng’ –English Dictionary (2003) iliteuliwa kama msingi wa uchun...
Nafasi ya Ikolojia ya Lugha katika Mtagusano wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Dini katika Kaunti ya Bungoma
Nafasi ya Ikolojia ya Lugha katika Mtagusano wa Kiswahili na Kibukusu katika Mawanda ya Dini katika Kaunti ya Bungoma
Nyanja mbalimbali katika jamii hutegemea matumizi ya lugha. Hali hii huzua changamoto ya namna ya kutumia raslimali za lugha zinazopatikana katika jamiilugha fulani. Juhudi ya kufa...
Muundo wa Kifonolojia wa Maneno ya Sheng’
Muundo wa Kifonolojia wa Maneno ya Sheng’
Utafiti huu ulidhamiria kutathmini athari za kamusi ya Sheng’ – English Dictionary kwa Kiswahili sanifu. Kamusi ya Sheng’ – English Dictionary (2003) iliteuliwa kama msingi wa uchu...
Athari za Mtaala wa Umilisi katika Ukuzaji wa Umahiri wa Kuzungumza Kiswahili kwa Wanafunzi wa Shule za Sekondari Nchini Uganda
Athari za Mtaala wa Umilisi katika Ukuzaji wa Umahiri wa Kuzungumza Kiswahili kwa Wanafunzi wa Shule za Sekondari Nchini Uganda
Umahiri wa kuzungumza lugha ni miongoni mwa matokeo yanayotarajiwa kutoka kwa mtu yeyote anayejifunza lugha ya kigeni au lugha ya pili. Mathalani nchini Uganda imebainika kuwa kiwa...
Ujitokezaji wa Viarudhi vya Kifonolojia katika Kihaya: Uchunguzi Kifani wa Toni katika Lahaja ya Kihamba
Ujitokezaji wa Viarudhi vya Kifonolojia katika Kihaya: Uchunguzi Kifani wa Toni katika Lahaja ya Kihamba
Fonolojia ni taaluma iliyosheheni viarudhi au vipambasauti kama ambavyo wataalamu wengine huviita. Miongoni mwake ni toni, lafudhi, mkazo, nguvumsikiko, usilabi, kiimbo, unguvunguv...
Utabirifu wa Makosa ya Utenganishaji na Uunganishaji wa Maneno katika Kiswahili
Utabirifu wa Makosa ya Utenganishaji na Uunganishaji wa Maneno katika Kiswahili
Uandishi ni mchakato unaohitaji umakini ili kinachoandikwa kieleweke kwa msomaji kwa namna iliyokusudiwa na mwandishi. Ikiwa kueleweka kutazingatiwa, basi, kutakuwa na mawasiliano ...
Utabirifu wa Makosa ya Utenganishaji na Uunganishaji wa Maneno katika Kiswahili
Utabirifu wa Makosa ya Utenganishaji na Uunganishaji wa Maneno katika Kiswahili
Uandishi ni mchakato unaohitaji umakini ili kinachoandikwa kieleweke kwa msomaji kwa namna iliyokusudiwa na mwandishi. Ikiwa kueleweka kutazingatiwa, basi, kutakuwa na mawasiliano ...

Back to Top