Search engine for discovering works of Art, research articles, and books related to Art and Culture
ShareThis
Javascript must be enabled to continue!

Mchango wa Ujumi Mweusi katika Unusura wa Nyimbo za Muziki wa Dansi wa Tanzania: 1970- 2000

View through CrossRef
Nyimbo za muziki wa dansi wa Tanzania zilianza nchini Tanzania kipindi cha ukoloni. Nyimbo hizi zinasawiri ujumi mweusi kwa kiasi kikubwa, na zina unusura. Ujumi wa kijamii huwa na dhima muhimu katika kazi za kifasihi za jamii husika. Kila jamii ina ujumi wake. Ujumi wa Waafrika huitwa ujumi mweusi. Huu ni ujumi utokanao na utamaduni wa jamii ya Kiafrika pamoja na mazingira yake. Ujumi huu huweza kutumika kuhakikia kazi za kifasihi za Kiafrika. Makala hii imetumia data za maktabani. Jumla ya nyimbo 8 za kuanzia mwaka 1970-2000 zimetumika. Nyimbo hizo zimeteuliwa kimakusudi, kwa kutumia usampulishaji usonasibu. Uteuzi huo umefanywa kwa zingatia dhima kuu, na ya kipekee, inayojitokeza zaidi kwenye wimbo husika. Mbinu zilizotumika kukusanyia data ni; utazamaji makini, udurusu wa matini na mbinu ya kutalii na kukusanya. Data zimechambuliwa kwa kutumia mkabala wa kitaamuli, na nadharia ya Uhalisia imetumika katika uchambuzi wa data ya utafiti huu. Matokeo ya utafiti wa makala hii yanabainisha kwamba ujumi mweusi una mchango mkubwa katika unusura wa nyimbo teule. Unusura huo umebainika kusababishwa na usawiri, kwa mawanda mapana vipengele mbalimbali vya ujumi mweusi kwenye nyimbo teule. Vipengele hivyo ni; umoja na ushirika, adabu na utii, utu, na matumizi bora ya lugha ya Kiswahili. Hivyo, walengwa wake huvutika kuzisikiliza kwani hugusa mambo yanayojenga ustawi wa jamii yao, hivyo kuwa na unusura. Hivyo, wasanii wanashauriwa kuendelea kutunga nyimbo za muziki wa dansi wa Tanzania zenye usawiri wa ujumi mweusi kwa mawanda mapana. Hali hii itasaidia kuendeleza unusura wa nyimbo hizi, kwa ajii ya usatawi wa jamii ya Watanzania na jamii nyinginezo
East African Nature and Science Organization
Title: Mchango wa Ujumi Mweusi katika Unusura wa Nyimbo za Muziki wa Dansi wa Tanzania: 1970- 2000
Description:
Nyimbo za muziki wa dansi wa Tanzania zilianza nchini Tanzania kipindi cha ukoloni.
Nyimbo hizi zinasawiri ujumi mweusi kwa kiasi kikubwa, na zina unusura.
Ujumi wa kijamii huwa na dhima muhimu katika kazi za kifasihi za jamii husika.
Kila jamii ina ujumi wake.
Ujumi wa Waafrika huitwa ujumi mweusi.
Huu ni ujumi utokanao na utamaduni wa jamii ya Kiafrika pamoja na mazingira yake.
Ujumi huu huweza kutumika kuhakikia kazi za kifasihi za Kiafrika.
Makala hii imetumia data za maktabani.
Jumla ya nyimbo 8 za kuanzia mwaka 1970-2000 zimetumika.
Nyimbo hizo zimeteuliwa kimakusudi, kwa kutumia usampulishaji usonasibu.
Uteuzi huo umefanywa kwa zingatia dhima kuu, na ya kipekee, inayojitokeza zaidi kwenye wimbo husika.
Mbinu zilizotumika kukusanyia data ni; utazamaji makini, udurusu wa matini na mbinu ya kutalii na kukusanya.
Data zimechambuliwa kwa kutumia mkabala wa kitaamuli, na nadharia ya Uhalisia imetumika katika uchambuzi wa data ya utafiti huu.
Matokeo ya utafiti wa makala hii yanabainisha kwamba ujumi mweusi una mchango mkubwa katika unusura wa nyimbo teule.
Unusura huo umebainika kusababishwa na usawiri, kwa mawanda mapana vipengele mbalimbali vya ujumi mweusi kwenye nyimbo teule.
Vipengele hivyo ni; umoja na ushirika, adabu na utii, utu, na matumizi bora ya lugha ya Kiswahili.
Hivyo, walengwa wake huvutika kuzisikiliza kwani hugusa mambo yanayojenga ustawi wa jamii yao, hivyo kuwa na unusura.
Hivyo, wasanii wanashauriwa kuendelea kutunga nyimbo za muziki wa dansi wa Tanzania zenye usawiri wa ujumi mweusi kwa mawanda mapana.
Hali hii itasaidia kuendeleza unusura wa nyimbo hizi, kwa ajii ya usatawi wa jamii ya Watanzania na jamii nyinginezo.

Related Results

Mabadiliko katika Mtaala wa Elimu ya Msingi na Namna Yanavyoathiri Tathmini katika Elimu ya Juu
Mabadiliko katika Mtaala wa Elimu ya Msingi na Namna Yanavyoathiri Tathmini katika Elimu ya Juu
Makala haya yamekusudia kuchunguza namna ambavyo mabadiliko katika mtaala wa elimu ya msingi yanavyoathiri tathmini katika elimu ya juu. Mabadiliko ya mtaala yanafanyika katika nga...
Jinsi Masuala ya Kijinsia Yalivyo Shughulikiwa Katika Tamthilia ya ‘Bembea ya Maisha’ kwa Kuzingatia Jinsia ya Mwandishi
Jinsi Masuala ya Kijinsia Yalivyo Shughulikiwa Katika Tamthilia ya ‘Bembea ya Maisha’ kwa Kuzingatia Jinsia ya Mwandishi
Maumbile ya binadamu yamechukua mikondo miwili; mwanamume na mwanamke. Jamii tofauti hutoa majukumu kwa kuzingatia migao hii miwili. Hivi ni kusema kuwa, shughuli za mtu katika jam...
Uambikaji wa Viambishi Ngeli katika Nomino Sahili Zinazorejelea Ndugu na Maana yake katika Sarufi ya Kiswahili
Uambikaji wa Viambishi Ngeli katika Nomino Sahili Zinazorejelea Ndugu na Maana yake katika Sarufi ya Kiswahili
Nomino sahili ni maneno ambayo kimofolojia yameundwa na mofu huru moja. Pia, kisematiki, maneno haya yana maana zake katika kamusi. Licha ya kuwa na sifa hizi, uambikaji wa viambis...
Mchango wa Mikakati ya Upole Katika Mazungumzo ya ibada ya Mazishi katika Lugha ya Kikabrasi
Mchango wa Mikakati ya Upole Katika Mazungumzo ya ibada ya Mazishi katika Lugha ya Kikabrasi
Swahili Suala la upole limetafitiwa na wasomi wengi kwenye mawasiliano, ikiwemo mazungumzo ya abiria na wahudumu wa magari ya uchukuzi kwa lugha ya Kikamba. Hata hivyo, utafiti huu...
Matumizi ya Lugha Kwenye Malezi ya Watoto: Mfano wa Matumizi ya Semi Katika Jamii ya Wamasaaba Nchini Uganda
Matumizi ya Lugha Kwenye Malezi ya Watoto: Mfano wa Matumizi ya Semi Katika Jamii ya Wamasaaba Nchini Uganda
Katika makala haya, mtafiti anaeleza jinsi lugha inavyotumiwa na wazazi katika shughuli yao ya kulea watoto. Alifanya hivyo kwa kurejelea malezi ya watoto katika jamii ya Wamasaaba...
Matumizi ya Lugha katika Tamthiliya ya ( Sadaka ya John Okello )
Matumizi ya Lugha katika Tamthiliya ya ( Sadaka ya John Okello )
Kipengele hiki hakipatikani katika lugha zote (bonyeza chache tu). Grafu iliyotangulia Ni ngapi huduma hii haipatikani katika lugha zote. Chini ni orodha ya kurasa zetu maarufu za ...
Mikakati ya Upole Katika Mawasiliano ya Wahudumu wa Magari ya Uchukuzi na Abiria katika lugha ya Kikamba.
Mikakati ya Upole Katika Mawasiliano ya Wahudumu wa Magari ya Uchukuzi na Abiria katika lugha ya Kikamba.
Upole ni hali ya msemaji kudhihirisha kuwa anajali hisia na mahitaji ya msikilizaji katika mazungumzo. Mikakati ya upole hutumiwa na washiriki wa mazungumzo kulainisha na kufanikis...
Athari ya Mitindo Mbalimbali ya Breili katika Unukuzi wa Maandishi ya Breili ya Kiswahili
Athari ya Mitindo Mbalimbali ya Breili katika Unukuzi wa Maandishi ya Breili ya Kiswahili
Utafiti huu ulinuia kuchanganua usahihi wa unukuzi wa maandishi ya breili hadi maandishi ya kawaida na kinyume chake, ili kuleta maana iliyokusudiwa. Katika kutimiza lengo hilo, ut...

Back to Top