Javascript must be enabled to continue!
Vipengele Vya Ontolojia Katika Tamthiliya Za Kiswahili: Mashetani (1971) Na Kivuli Kinaishi (1990).
View through CrossRef
Makala haya yalilenga kuchambua vipengele vya Ontolojia ya Kiafrika katika tamthiliya za Kiswahili: mfano wa Mashetani (1971) na Kivuli Kinaishi (1990). Mbinu iliyotumika katika kukusanya data hii ni mbinu ya kitaamuli. Sampuli iliyotumika katika makala haya ni vitabu viwili vya tamthiliya ambavyo ni Mashetani (1971) na Kivuli Kinaishi (1990). Tamthiliya hizi zitawakilisha zingine nyingi ambazo zimeandikwa na Ibrahimu Hussein na Said Mohamed. Mtafiti atajikita katika tamthiliya hizo mbili ili kuchambua vipengele vya ontolojia. Utafiti huu ulifanywa maktabani ambapo data ziliweza kukusanywa kwa kutumia mbinu ya udurusu maktaba. Mtafiti alipitia maandishi mbalimbali kutoka katika vitabu vilivyopo katika maktaba pamoja na wavuti ili kupata maelezo yaliyotosha kukidhi haja ya makala haya. Utafiti huu uliongozwa na Nadharia ya Ontolojia ambapo mtafiti aliitumia katika kuchambua vipengele vya ontolojia ya Kiafrika katika tamthiliya teule. Makala haya yatasaidia kuongeza uelewa kwa wanajamii hasa kwa wale wasiofahamu kuchambua masuala ya kiontolojia katika fasihi andishi. Kutokana na matokeo ya utafiti huu tumefikia mahitimisho kuwa vipengele vya ontolojia ya Kiafrika vilivyobainishwa kutoka katika tamthiliya ya Mashetani na Kivuli Kinaishi vimeweza kusawiri ontolojia ya Kiafrika na nafasi yake kwa jamii.
Editon Consortium Publishing
Title: Vipengele Vya Ontolojia Katika Tamthiliya Za Kiswahili: Mashetani (1971) Na Kivuli Kinaishi (1990).
Description:
Makala haya yalilenga kuchambua vipengele vya Ontolojia ya Kiafrika katika tamthiliya za Kiswahili: mfano wa Mashetani (1971) na Kivuli Kinaishi (1990).
Mbinu iliyotumika katika kukusanya data hii ni mbinu ya kitaamuli.
Sampuli iliyotumika katika makala haya ni vitabu viwili vya tamthiliya ambavyo ni Mashetani (1971) na Kivuli Kinaishi (1990).
Tamthiliya hizi zitawakilisha zingine nyingi ambazo zimeandikwa na Ibrahimu Hussein na Said Mohamed.
Mtafiti atajikita katika tamthiliya hizo mbili ili kuchambua vipengele vya ontolojia.
Utafiti huu ulifanywa maktabani ambapo data ziliweza kukusanywa kwa kutumia mbinu ya udurusu maktaba.
Mtafiti alipitia maandishi mbalimbali kutoka katika vitabu vilivyopo katika maktaba pamoja na wavuti ili kupata maelezo yaliyotosha kukidhi haja ya makala haya.
Utafiti huu uliongozwa na Nadharia ya Ontolojia ambapo mtafiti aliitumia katika kuchambua vipengele vya ontolojia ya Kiafrika katika tamthiliya teule.
Makala haya yatasaidia kuongeza uelewa kwa wanajamii hasa kwa wale wasiofahamu kuchambua masuala ya kiontolojia katika fasihi andishi.
Kutokana na matokeo ya utafiti huu tumefikia mahitimisho kuwa vipengele vya ontolojia ya Kiafrika vilivyobainishwa kutoka katika tamthiliya ya Mashetani na Kivuli Kinaishi vimeweza kusawiri ontolojia ya Kiafrika na nafasi yake kwa jamii.
Related Results
Vikwazo vya Usimilishaji wa Ishara za Isimu katika Breili
Vikwazo vya Usimilishaji wa Ishara za Isimu katika Breili
Utafiti huu ulinuia kuchanganua usimilishaji wa ishara za isimu katika breili ya Kiswahili. Uchanganuzi huu ulitiwa hamasa na mambo matano muhimu. Kwanza, breili ndio njia ya pekee...
Athari ya Ukosefu wa Ishara za Isimu katika Ufundishaji na Athari ya Mikato ya Kiingereza na Kiswahili katika Uchapishaji wa Vitabu
Athari ya Ukosefu wa Ishara za Isimu katika Ufundishaji na Athari ya Mikato ya Kiingereza na Kiswahili katika Uchapishaji wa Vitabu
Utafiti huu ulinuia kuchanganua usimilishaji wa ishara za isimu katika breili ya Kiswahili. Uchanganuzi huu ulitiwa hamasa na mambo matano muhimu. Kwanza, breili ndio njia ya pekee...
Uraia, Lugha na Haki za Kidijitali: umuhimu wa lugha katika harakati za kuondoa ukoloni katika teknolojia
Uraia, Lugha na Haki za Kidijitali: umuhimu wa lugha katika harakati za kuondoa ukoloni katika teknolojia
Purpose
Maneno mengi yanayohusu haki za binadamu na haki za kiteknolojia hayajatafsiriwa katika lugha ya Kiswahili. Kwa hivyo, wataalamu wa teknolojia na watetezi wa haki za kidiji...
Vipengele Vya Fasihi Vinavyojenga Taswira Ya Mwanamke Katikavitabu Teule Vya Biblia Takatifu
Vipengele Vya Fasihi Vinavyojenga Taswira Ya Mwanamke Katikavitabu Teule Vya Biblia Takatifu
Lugha ni chombo cha kipekee kinachofinyangwa kuwasilisha taswira ya masuala changamano katika jamii. Matokeo haya ya lugha ni fasihi, ambayo ni kioo cha jamii. Biblia Takatifu ni k...
Uchunguzi wa Dhamira Zinazojengwa na Vipengele vya Sanaa katikaVisasuli vya Wahaya
Uchunguzi wa Dhamira Zinazojengwa na Vipengele vya Sanaa katikaVisasuli vya Wahaya
Sanaa ni sehemu muhimu ya maisha ya kila siku katika kabila la Wahaya. Umuhimu wa sanaa katika kabila la Wahaya unatokana na utajiri mkubwa walionao katika fasihi simulizi hususani...
Usahihi wa Uhawilishaji wa Viwakilishi vya Jinsia katika Vitabu vya Kiingereza Vilivyotafsiriwa kutoka Kiswahili
Usahihi wa Uhawilishaji wa Viwakilishi vya Jinsia katika Vitabu vya Kiingereza Vilivyotafsiriwa kutoka Kiswahili
Kusudi: Utafiti huu ulichunguza usahihi wa uhawilishaji wa viwakilishi vya jinsia katika vitabu vya Kiingereza vilivyotafsiriwa kutoka Kiswahili kwenda Kiingereza. Utafiti huu ulid...
Ubainishaji wa Vipengele vya Ujumi wa Kiafrika na Athari yake katika Ushairi wa Kiswahili: Uchunguzi wa Ushairi wa Bongo Fleva
Ubainishaji wa Vipengele vya Ujumi wa Kiafrika na Athari yake katika Ushairi wa Kiswahili: Uchunguzi wa Ushairi wa Bongo Fleva
Makala haya yalichunguza ujitokezaji wa ujumi wa Kiafrika katika ushairi wa Kiswahili wa Bongo Fleva pamoja na athari yake katika ushairi huo. Tafiti kuhusu vipengele vya ujumi wa ...
Ushairi WA Kiganda Unavyoweza Kuchangia Na Kuendeleza Ushairi WA Kiswahili Kimtindo Na Kimaudhui: Mfano WA Ufundishaji Nchini Uganda
Ushairi WA Kiganda Unavyoweza Kuchangia Na Kuendeleza Ushairi WA Kiswahili Kimtindo Na Kimaudhui: Mfano WA Ufundishaji Nchini Uganda
Wanafunzi wengi nchini Uganda wanachukulia utanzu wa ushairi wa Kiswahili kuwa mgumu na wanapata ugumu katika kujifunza ushairi wa Kiswahili. Ushairi wa Kiganda umekuwa unatendwa v...

