Javascript must be enabled to continue!
Ushairi wa Simu Tamba wa Waswahili wa Pwani ya Kenya
View through CrossRef
Katika makala hii tunajadili jinsi simu tamba inavyotumika kama nyenzo katika uandishi, ukuzaji na usambazaji wa ushairi miongoni mwa Waswahili wa Pwani ya Kenya na hatimaye watu wengine kote ulimwenguni. Ili kutimiza malengo haya tumetumia dhana ya utandawazi kama dhana changanuzi na vilevile Nadharia ya Kisosholojia ya Kiuhakiki lli kuchambua masuala ya kimaudhui ya ushairi wa simu tamba. Data ya utafiti huu imekusanywa kutokana na kutangamana na jumuiya ya Waswahili wa Pwani ya Kenya kupitia simu tamba. Mmoja wa waandishi wa kazi hii pia ni Mswahili wa Pwani ya Kenya na mshiriki katika mitagusano hii ya ushairi wa simu tamba. Katika kazi hii tumeangazia maudhui ya ushairi wa simu tamba miongoni mwa Waswahili wa Pwani ya Kenya na vilevile kuonesha baadhi ya mitindo inayopendelewa katika ushairi huu. Imebainika kuwa maudhui ya ushairi wa simu tamba katika eneo la Pwani ya Kenya yanahusu salamu za kutakiana heri siku ya Ijumaa na wakati wa mfungo wa Ramadhani. Masuala mengine ya kijamii yanayojitokeza ni yale yanayofungamana na ndoa, dini, uchumi na siasa. Imedhihirika pia kuwa mashairi ya simu tamba yanatungwa kwa kuzingatia kanuni za kijadi kama vile kuwa na urari wa vina, kupangilia shairi kwa kutumia beti, kuwa na mishororo iliyokadiriwa, na kuwa na urari wa vina na mizani. Mengi ya mashairi ya Waswahili wa Pwani ya Kenya ni ya muundo wa tathlitha na tarbia. Hata hivyo, kuna changamoto za kutunga na kuuendeleza ushairi wa Kiswahili kwa njia ya simu tamba kama vile ugumu wa kupangilia mishororo na hata vipande vya mashairi kwa namna inayofungamana na arudhi.
Title: Ushairi wa Simu Tamba wa Waswahili wa Pwani ya Kenya
Description:
Katika makala hii tunajadili jinsi simu tamba inavyotumika kama nyenzo katika uandishi, ukuzaji na usambazaji wa ushairi miongoni mwa Waswahili wa Pwani ya Kenya na hatimaye watu wengine kote ulimwenguni.
Ili kutimiza malengo haya tumetumia dhana ya utandawazi kama dhana changanuzi na vilevile Nadharia ya Kisosholojia ya Kiuhakiki lli kuchambua masuala ya kimaudhui ya ushairi wa simu tamba.
Data ya utafiti huu imekusanywa kutokana na kutangamana na jumuiya ya Waswahili wa Pwani ya Kenya kupitia simu tamba.
Mmoja wa waandishi wa kazi hii pia ni Mswahili wa Pwani ya Kenya na mshiriki katika mitagusano hii ya ushairi wa simu tamba.
Katika kazi hii tumeangazia maudhui ya ushairi wa simu tamba miongoni mwa Waswahili wa Pwani ya Kenya na vilevile kuonesha baadhi ya mitindo inayopendelewa katika ushairi huu.
Imebainika kuwa maudhui ya ushairi wa simu tamba katika eneo la Pwani ya Kenya yanahusu salamu za kutakiana heri siku ya Ijumaa na wakati wa mfungo wa Ramadhani.
Masuala mengine ya kijamii yanayojitokeza ni yale yanayofungamana na ndoa, dini, uchumi na siasa.
Imedhihirika pia kuwa mashairi ya simu tamba yanatungwa kwa kuzingatia kanuni za kijadi kama vile kuwa na urari wa vina, kupangilia shairi kwa kutumia beti, kuwa na mishororo iliyokadiriwa, na kuwa na urari wa vina na mizani.
Mengi ya mashairi ya Waswahili wa Pwani ya Kenya ni ya muundo wa tathlitha na tarbia.
Hata hivyo, kuna changamoto za kutunga na kuuendeleza ushairi wa Kiswahili kwa njia ya simu tamba kama vile ugumu wa kupangilia mishororo na hata vipande vya mashairi kwa namna inayofungamana na arudhi.
Related Results
Ushairi WA Kiganda Unavyoweza Kuchangia Na Kuendeleza Ushairi WA Kiswahili Kimtindo Na Kimaudhui: Mfano WA Ufundishaji Nchini Uganda
Ushairi WA Kiganda Unavyoweza Kuchangia Na Kuendeleza Ushairi WA Kiswahili Kimtindo Na Kimaudhui: Mfano WA Ufundishaji Nchini Uganda
Wanafunzi wengi nchini Uganda wanachukulia utanzu wa ushairi wa Kiswahili kuwa mgumu na wanapata ugumu katika kujifunza ushairi wa Kiswahili. Ushairi wa Kiganda umekuwa unatendwa v...
Uathirianomatini wa Kimtindo katika Ushairi wa Kiswahili: Mfano wa “Utenzi wa Hati” na “Utenzi wa Mwanakupona”
Uathirianomatini wa Kimtindo katika Ushairi wa Kiswahili: Mfano wa “Utenzi wa Hati” na “Utenzi wa Mwanakupona”
Bakhtin (1981) anaeleza kwamba matini za kifasihi huathiriana na kuhusiana. Kila matini ya kifasihi ina sauti zinazoingiliana na kuhusiana na matini nyingine zilizopo, zilizopita a...
LOAN RECOVERY OF HIGHER EDUCATION LOANS
LOAN RECOVERY OF HIGHER EDUCATION LOANS
Higher Education Loans Board (HELB) is the major source of financing higher education in Kenya. Non-repayment of the loan among university students after they have graduated is a m...
Resistance levels of cassava landraces to CMD, CBSD and vector whiteflies in Malawi
Resistance levels of cassava landraces to CMD, CBSD and vector whiteflies in Malawi
Abstract
Cassava mosaic disease (CMD) and cassava brown streak disease (CBSD) have been two major threats to cassava production in eastern and southern Africa. This study w...
MIKOKO: A Data Sharing Platform On Kenyan Mangrove Species
MIKOKO: A Data Sharing Platform On Kenyan Mangrove Species
The Mangrove ecosystem offers a range of benefits and opportunities for local and national economic development such as fisheries, shoreline stability, and resource sustainability ...
Strategi Pemenangan Politik Tamba-Ipat dalam Pilkada Kabupaten Jembrana Tahun 2020
Strategi Pemenangan Politik Tamba-Ipat dalam Pilkada Kabupaten Jembrana Tahun 2020
Penelitian ini mengelaborasi strategi pemenangan pasangan calon Tamba-Ipat dalam kontestasi Pilkada Kabupaten Jembrana Bali tahun 2020 dengan teoristrategi marketing politik 3P Adm...
Tamba and Damphu in Tambakaiten as the Network of Tamang and Songs
Tamba and Damphu in Tambakaiten as the Network of Tamang and Songs
Santabir Lama’s Tamba Kaiten is a cultural documentation of Tamang community focusing especially in central region of Nepal, about cultural and religious rites and rituals through ...
Effect of Fintech Services on Financial Inclusion in Kenya
Effect of Fintech Services on Financial Inclusion in Kenya
Abstract
Many research studies have been done to investigate the subject of financial inclusion. However, there has been no recent study on the impact of FinTechs on Financ...

